Nav bar

Jumatano, 16 Oktoba 2024

NWM-DKT. BITEKO: ASILIMIA 55 YA KAYA NCHINI ZINAFANYA SHUGHULI ZA UFUGAJI KUKU

Na. Stanley Brayton

Naibu Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Dotto Biteko amesema asilimia 55 ya kaya nchini zinafanya shughuli za ufugaji kuku uliopelekea ongezeko la uchumi jumuishi unaolenga kujenga kesho iliyo bora.

Amyasema hayo leo tarehe 16 Oktoba, 2024 katika ukumbi wa Serena Hotel Dar Es Salaam wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Jukwaa la Tasnia ya Kuku na Ndege wafugwao kwa Nchi za Kusini mwa Afrika.

“Tasnia hii imeajiri zaidi wanawake na vijana, vilevile inazalisha malighafi za viwanda, inachangia usalama wa chakula na lishe na upatikanaji wa fedha za kigeni” 

Aidha Dkt. Bitteko amesema lengo la mkutano huo ni kujadili na kubadilishana uzoefu kutoka nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), pamoja na kubainisha fursa za kimkakati zinazohusu tasnia ya kuku na ndege wafugwao.

Naye, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Abdallah Ulega amesema kuwa kuku ni mifugo rafiki na mifugo hiyo haihitaji eneo kubwa katika kuitunza, inazaliana kwa haraka na haihitaji mtaji mkubwa hivyo mikakati ya uwekezaji katika Tasnia hiyo ili kuongeza ajira hususani kwa Vijana na Wanawake na kuhangia pato la taifa,

Aidha ametoa wito kwa wadau mbalimbali kushirikiana na Wizara yenye dhamana ya Mifugo na Uvuvi kipindi wanapofanya tafiti zinazohusu mifugo na uvuvi na mazao yake ili kuepusha kuleta taharuki kwa watumiaji wa bidhaa hizo.


Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko, akihutubia washiriki (hawapo pichani) wa Jukwaa la Tasnia ya kuku na ndege wafugwao ambalo limefanyika Hoteli ya Serena, Oktoba 16, 2024. Dar es Salaam


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Hamis Ulega, akihutubia washiriki (hawapo pichani) wa Jukwaa la Tasnia ya kuku na ndege wafugwao ambalo limefanyika Hoteli ya Serena, Oktoba 16, 2024. Dar es Salaam


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, akizungumza na washiriki (hawapo pichani) wa Jukwaa la Tasnia ya kuku na ndege wafugwao ambalo limefanyika Hoteli ya Serena, Oktoba 16, 2024. Dar es Salaam


Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (aliekaa katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na Mashirika ya Binafsi, ni katika Jukwaa la Tasnia ya kuku na ndege wafugwao, lililofanyika katika Hoteli ya Serena, Oktoba 16, 2024. Dar es Salaam. Wa pili kulia kwa waliokaa ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Hamis Ulega


Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati, Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (aliekaa katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na vijana wa mnyororo wa thamani katika Tasnia ya kuku kutoka nchi Tanzania (62), Msumbiji (10) na Shirikisho la Vyama vya Kilimo Kusini mwa Afrika SACAU (10) ambao wamepongezwa leo kwa mchango wao katika Tasnia hiyo, ni katika Jukwaa la Tasnia ya kuku na ndege wafugwao, lililofanyika katika Hoteli ya Serena, Oktoba 16, 2024. Dar es Salaam. Wa pili kulia kwa waliokaa ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Hamis Ulega


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni