Nav bar

Jumatano, 9 Oktoba 2024

DKT. MPANGO AZIPONGEZA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI KWA UTEKELEZAJI MZURI WA SHUGHULI ZAKE

Na. Stanley Brayton

Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, amezipongeza Sekta za Mifugo na Uvuvi kwa utekelezaji mzuri wa shughuli zake ambazo zimelenga kukuza shughuli za ufugaji na uvuvi kwa kuendana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika kuhudumia wananchi na kuwapa maisha Bora.

Akizungumza, Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango leo Oktoba 8, 2024 katika Ziara yake wilayani Igunga, Mkoani Tabora, Dkt. Mpango amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi inafanya vizuri katika kuhakikisha mifugo bora inapatikana kwa wananchi kwa kutoa pembejeo bora kwa wafugaji na wavuvi, vilevile kutoa mikopo kwa wafugaji na wavuvi pamoja na kuwapatia mbegu bora za vifaranga vya samaki pamoja na madume Bora ya ng'ombe.

Kwa Upande wake, Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti amesema Serikali kupitia Wizara ya Mifugo imefanya mambo mengi sana kwa watanzania na ata katika Wilaya ya Igunga ikiwa ni kutoa elimu kwa wafugaji na wavuvi.

“tuna fursa ya ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba, na ya utengenezaji wa mabwawa ya kufugia samaki pamoja na kutoa madume Bora ya ng'ombe kama mbegu”, amesema Mhe. Mnyeti

Aidha, Mhe. Mnyeti amesema, Madume Bora ya ng'ombe yalishagawiwa katika baadhi ya wilaya, ikiwemo Wilaya ya Bahi, Serengeti na Bunda.

Vilevile, Mhe. Mnyeti amesema mpango huo ni endelevu hapa nchini, na Wizara inampango wa kusambaza madume hayo Bora ya ng'ombe katika wilaya zote nchini Tanzania ila yaweze kupanda ng'ombe wa kienyeji na kupata ng'ombe wengine walio Bora.


Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, akimuuliza swali Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti (hayupo pichani), ni lini Wizara italeta Madume Bora ya ng'ombe Wilayani Igunga, ni katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Igunga - Tabora


Naibu Waziri Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti, akijibu swali la Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpangoni (hayupo pichani), kuwa Wizara italeta Madume Bora ya ng'ombe 20 Wilayani Igunga baada ya wiki tatu, ni katika Ziara ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Igunga - Tabora


Picha ni wananchi wakimsikiliza Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora ya Oktoba 8, 2024, Igunga - Tabora


Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, akizungumza na wananchi wa kijiji cha Bukene kuhusu umuhimu wa kuzingatia lishe Bora kwa watoto na mama wajawazito ili waweze pata Protini ya kutosha itakayowasaidia kukuza ufikiri wa mtoto na kusisitiza Maafisa kutoa elimu kuhusu lishe Bora ili jamii zielewe nini maana ya lishe bora na umuhimu wake, ni katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora


Naibu Waziri Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti, akisalimia wanakijiji wa Bukene na kutoa Salamu za Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ni katika Ziara ya kikazi Mkoani Tabora ya Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora



 Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango (aliyeshika bomba la maji), akifungua maji kama Ishara ya Uzinduzi  na Upanuzi wa Mradi wa Maji kutoka ziwa Viktoria kwenda Bukene, ni katika Ziara yake ya kikazi Mkoani Tabora, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora, Wa tatu kulia ni Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti


Picha ni Washiriki mbalimbali wakiwemo wakazi wa Bukene na Maafisa mbalimbali na Viongozi wa Serikali wakiwa katika Ziara ya kikazi Mkoani Tabora ya Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, Oktoba 8, 2024, Nzega - Tabora





Hakuna maoni:

Chapisha Maoni