Nav bar

Jumamosi, 30 Septemba 2023

ULEGA AKIWAHUTUBIA WANAJUMUIYA YA WAISLAMU WA SUNNI KATIKA TUKIO LA KUADHIMISHA SIKUKUU YA KUZALIWA BWANA MTUME MUHAMMAD (S.A.W)

 


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akiwahutubia Wanajumuiya ya Waislamu wa Sunni katika tukio la kuadhimisha Sikukuu ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) liliyofanyika katika Msikiti wa Sunni jijini Dar es Salaam usiku wa Septemba 28, 2023. Katika tukio hilo, Waziri Ulega ndiye alikuwa mgeni rasmi akimuwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katikati) akiwa  na aliyewahi kuwa Shekhe wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum (kulia) wakishuhudia matukio mbalimbali yaliyokuwa yakiendelea katika sherehe ya maadhimisho ya Sikukuu ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) iliyofanyika katika Msikiti wa Sunni jijini Dar es Salaam usiku wa Septemba 28, 2023.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (kushoto) akifurahia jambo na Mbunge wa Jimbo la Mpendae, Zanzibar, Mhe. Taufiq Turki walipokutana katika tukio la kuadhimisha Sikukuu ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) liliyofanyika katika Msikiti wa Sunni jijini Dar es Salaam usiku wa Septemba 28, 2023.

Sehemu ya Viongozi wa Jumuiya ya Waislamu wa Sunni wakiwa katika meza kuu katika tukio la kuadhimisha Sikukuu ya kuzaliwa Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) liliyofanyika katika Msikiti wa Sunni jijini Dar es Salaam usiku wa Septemba 28, 2023.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni