Nav bar

Jumatano, 31 Mei 2023

SEKTA YA UVUVI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA SHIRIKA LA MAENDELEO LA KIMATAIFA LA JAPAN (JICA)

 

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani (Sekta ya Uvuvi) kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh pamoja na viongozi wengine wa TAFIRI na wizara hiyo, kwenye mazungumzo ya kuendeleza ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), ambapo baadhi ya maafisa waandamizi wa shirika hilo hapa nchini walifika katika ofisi za makao makuu ya TAFIRI jijini Dar es Salaam ili kupata taarifa mbalimbali za TAFIRI na maeneo ya kushirikiana. (19.05.2023).


Maafisa waandamizi kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) hapa nchini, wakiwa kwenye mazungumzo na uongozi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) na baadhi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, mara baada ya maafisa hao kutoka JICA kufika makao makuu ya TAFIRI jijini Dar es Salaam ili kujadili maeneo ya kushirikiana katika Sekta ya Uvuvi na kupata taarifa mbalimbali juu ya taasisi hiyo. (19.05.2023).


Maafisa waandamizi kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) hapa nchini, mara baada ya mazungumzo na uongozi wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) na baadhi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwenye makao makuu ya TAFIRI jijini Dar es Salaam, juu ya kuendeleza ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi walipata fursa ya kujionea baadhi ya vifaa vya utafiti wa uvuvi (19.05.2023).


Picha ya pamoja ya Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) Dkt. Ismael Kimirei (wa tatu kutoka kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani (Sekta ya Uvuvi) kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh (wa pili kutoka kulia) na baadhi ya maafisa kutoka TAFIRI na wizara hiyo pamoja na maafisa waandamizi kutoka Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) hapa nchini, mara baada ya mazungumzo na uongozi wa TAFIRI na baadhi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi juu ya maeneo ya ushirikiano katika Sekta ya Uvuvi yaliyofanyika katika makao makuu ya TAFIRI jijini Dar es Salaam. (19.05.2023)


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni