Nav bar

Jumatano, 31 Agosti 2022

SERIKALI KUTOA MIKOPO KWA WAVUVI NA WAKUZAJI VIUMBE MAJI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amesema kuwa serikali imeandaa mpango wa kuwawezesha wavuvi na wakuzaji viumbe maji kwa kuwapatia mitaji ili waweze kuboresha shughuli zao.

 

Waziri Ndaki ameyasema hayo leo (30.08.2022) kwenye hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya wizara ya mifugo na uvuvi (sekta ya uvuvi) na benki ya maendeleo ya kilimo tanzania – TADB, hafla iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo katika Makao Makuu ya Jeshi la Magereza – Msalato Jijini Dodoma.

 

Mpango huu ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani katika hotuba yake aliyoitoa tarehe 07.01.2022 katika kilele cha Matembezi ya Miaka 58 ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo alisisitiza kutumika kwa fursa zilizopo katika kukuza Uchumi wa Buluu ikiwemo uvuvi na ukuzaji viumbe maji. Aidha, wakati akifunga Maonesho ya Sherehe za Wakulima (NANENANE), Mheshimiwa Rais aliagiza Wizara kuhakikisha kuwa uzalishaji wa Samaki unaongezeka kutoka tani 497,567 na kufikia tani 600,000 ifikapo mwaka 2025.

 

Katika utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais, Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeandaa Mpango wa kuwawezesha wavuvi na wakuzaji viumbe maji kwa kutoa mikopo isiyo na riba kwa vyama vya ushirika, vikundi vya wavuvi, wakuzaji viumbe maji, wavuvi binafsi na makampuni ya wavuvi. Mikopo hiyo itahusisha zana za kisasa za uvuvi ikiwemo boti, nyavu, injini, vizimba, vifaranga vya samaki, chakula cha samaki na pembejeo za ukulima wa mwani.

 

Waziri Ndaki ametoa wito kwa wavuvi na wakuzaji viumbe maji kuchangamkia fursa hiyo ya mikopo ili iweze kuwanufaisha. Aidha, amezisihi Halmashauri katika maeneo ya mradi kwenda kuwahamasisha wananchi wake ili waweze kuitumia kuitumia fursa hii ipasavyo.

 

Aidha, amemshukuru Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha shilingi bilioni 60 kwa ajili ya kuendeleza Sekta ya Uvuvi, fedha ambazo zipo katika bajeti ya mwaka 2022/2023. Waziri Ndaki amesema endapo zikitumika vizuri upo uwezekano mwaka ujao wa fedha fedha hizo zikaongezeka.

 

Waziri Ndaki amesema kama viongozi watahakikisha wanawasimamia wataalam wa Wizara kwa kuwa mradi huu unatakiwa kutakelezwa kwa muda maalum, hivyo ifikapo Juni 30, 2023 utekelezaji wa mradi huu uwe umekamilika.

 

Naye Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amesema kuwa kasi ya utoaji mikopo kwa wavuvi kupitia Benki ya Maendeleo ya Kilimo ni ndogo, kwani mahitaji ya watanzani, kasi ya kuwafiki na urahisi wa upataji mikopo bado ni mdogo. Hivyo TADB inayo kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha kwamba mikopo inafika kwa walengwa, kwani watu wengi wamehangaika kupata mikopo hasa wavuvi wadogo na kusababisha kukata tamaa na kuacha kufanya shughuli za uvuvi.

 

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma amesema kuwa Kamati imefurahishwa sana na mpango wa serikali wa kutoa mikopo isiyo na riba inayokwenda kuwasaidia wavuvi na wakuzaji viumbe maji. Mradi huu utakwenda kusaidia kuongeza uzalishaji wa samaki utakaokwenda kukidhi mahitaji makubwa yaliyopo.

 

Katibu Mkuu anayesimamia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Rashid Tamatamah amesema kuwa boti hizo zina urefu wa mita 7 hadi 14 zikiwa na injini zenye uwezo wa nguvu za farasi 9.9 hadi 60. Pia boti hizo zitakuwa na uwezo wa kubeba wavuvi 620, kubeba Samaki tani 1.5, mtambo wa kufuatilia/kutambua uwepo wa Samaki (Fish finder), kifaa cha kuongoza boti (GPS), vifaa vya kuokolea Maisha na zana za uvuvi zikijumuisha mishipi na nyavu. Jumla ya shilingi Bilioni 11.5 zimetengwa kwa ajili ya kukopeshwa na mkopo huo utalipwa kwa muda wa miaka mitano (5) bila Riba.

 

Wizara pia itatoa mkopo kwa Wafugaji Samaki kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kujenga jumla ya vizimba 831 ambapo kila kizimba kimoja kitakuwa na ukubwa wa mita za ujazo 144 M3 – 256 M3. Vilevile, itatoa jumla ya vifaranga 4,080,000 na chakula cha Samaki tani 3,482.5.

 

Aidha, mkataba huo uliosainiwa leo utahusisha wakulima wa mwani ambapo jumla ya wakulima 821 watakopeshwa kamba 108,372, tai tai 7,152,552 pamoja na mbegu za mwani. Kwa ujumla kiasi cha shilingi Bilioni 21 zitatumika kwa ajili ya vizimba na zao la mwani.

 

Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Frank Nyabudenge amesema kuwa benki hiyo ni taasisi ya kifedha ambayo ni benki ya serikali iliyojikita kwenye sekta ya kilimo. Moja ya malengo makubwa ya kuanzishwa kwake ni kuchangia utoshelevu wa chakula na usalama endelevu wa chakula nchini ambapo ni pamoja na utoaji lishe bora.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo Tanzania, Frank Nyabudenge (wa pili kulia wakisaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB). (30.08.2022)


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (Mb) akihutubia wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ambapo amesema kuwa Wizara imeandaa Mpango wa kuwawezesha wavuvi na wakuzaji viumbe maji kwa kutoa mikopo isiyo na riba kwa vyama vya ushirika, vikundi vya wavuvi, wakuzaji viumbe maji, wavuvi binafsi na makampuni ya wavuvi. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akitoa salam wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) ambapo amesema kuwa kasi ya utoaji mikopo kwa wavuvi kupitia TADB ni ndogo, kwani mahitaji ya watanzani, kasi ya kuwafiki na urahisi wa upataji mikopo bado ni mdogo, hivyo TADB inayo kazi kubwa ya kufanya ili kuhakikisha kwamba mikopo inawafikia walengwa kwa wakati. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30,08,2022)


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb) akitoa salam za kamati wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) amesema kuwa Kamati imefurahishwa sana na mradi huu wa kuwakopesha wavuvi na wakuzaji viumbe maji kwa kuwa utawasaidia kuongeza uzalisha na hivyo kuongeza upatikanaji wa samaki. Aidha, amesema kuwa Kamati itaendelea kuisimamia Wizara ili kuhakikisha maendeleo kwenye Sekta ya Uvuvi yanapatikana. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akitoa neno la utangulizi wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) amesema kuwa jumla ya wakulima 821 watakopeshwa kamba 108,372, tai tai 7,152,552 pamoja na mbegu za mwani. Kwa ujumla kiasi cha shilingi Bilioni 21 zitatumika kwa ajili ya vizimba na zao la mwani. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Naibu Katibu Mkuu, OR TAMISEMI (Afya), Dkt. Grace Magembe akitoa salam wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) amemuhakikishia Waziri kuwa TAMISEMI itashiriki kikamilifu kwenye mkakati huo kwa kuwa tayari wanayo mifumo ambayo ilikuwa ikitumika kwenye utoaji wa fedha. Hivyo watashirikiana na wataalam kutoka Sekta ya Uvuvi kuangalia ni wapi wanafanya vizuri na kama kutakuwa na changamoto ziweze kutatuliwa ili mradi huu uweze kuleta tija na matokeo yaliyotarajiwa. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Frank Nyabudenge akitoa salam za TADB wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) amesema kuwa watahakikisha mikopo hiyo inawafikia walengwa nakutoa matokeo chanya ya kuongeza mazao yatokanayo na uvuvi. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania, Frank Nyabudenge akitoa salam za TADB wakati wa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) amesema kuwa watahakikisha mikopo hiyo inawafikia walengwa nakutoa matokeo chanya ya kuongeza mazao yatokanayo na uvuvi. Hafla hii imefanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah (wa pili kushoto) na Mkurugenzi wa Benki ya Maendeleo Tanzania, Frank Nyabudenge (kulia) wakionyesha mikataba ya utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) mara baada ya kumaliza kusaini mikataba hiyo. (30.08.2022)


Picha ya pamoja ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (Mb), Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb), Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitenge wa Wizara hiyo mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)


Picha ya pamoja ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (Mb), Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (Mb), Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji, Mhe. Dkt. Christine Ishengoma (Mb), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah na Kamati ya maandalizi mara baada ya kumalizika kwa hafla ya kusaini mkataba wa utekelezaji wa mradi wa ununuzi wa boti za Uvuvi na vizimba vya kufugia samaki kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) iliyofanyika kwenye ukumbi wa Mzee uliopo Makao Makuu ya Jeshi la Magereza - Msalato Jijini Dodoma. (30.08.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni