Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2021

NDAKI: TUTABORESHA SEKTA YA MIFUGO KWA KUJENGA MAJOSHO 129

Picha
  SERIKALI imesema kuwa katika mwaka wa fedha 2021/22 imepanga kuboresha sekta ya mifungo ikiwa ni pamoja na kujenga majosho 129, ili kuongeza thamani ya bidhaa zitokanazo na mazao ya mifugo.   Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mashimba Ndaki, aliyasema hayo jana jijini Dodoma, wakati wizara yake ilipokuwa kiwasilisha bajeti ya sekta ya mifugo kwenye kamati ya kudumu ya bunge ya kilimo, mifugo na maji.   Alisema, Wizara hiyo imezamilia kufanya maboresho makubwa katika sekta ya mifugo ili kuongeza thamani ya mazao yatokanayo na mifugo na kuchangia katika pato la taifa.   Ndaki, alisema moja katika eneo ambalo watalifanyia kazi ni kujenga majosho 129, mapya pamoja na kukarabati yaliyopo ili kusaidia wafugaji kupata huduma hizo katika maeneo yao,   “Tutahakikisha kuwa tunajenga majosho kwa ajili ya kuogeshea mifugo kila eneo lenye mifugo nchini lakini pia kukarabati majosho yote yalipo ili kuwezesha wafugaji kupata huduma za ugani katika maeneo yao”alisema   Alisema, ...

MASHAMBA DARASA YA UFUGAJI SAMAKI KUANZISHWA KOTE NCHINI

Picha
Na. Edward Kondela   Serikali imesema katika bajeti ya mwaka wa fedha 2021/22 ina mpango wa kuanzisha vituo vya ukuzaji viumbe maji katika halmashauri 80 za wilaya ikiwa na lengo la kuhakikisha kila halmashauri inakuwa na kituo hicho ambacho kitatumika kama shamba darasa kwa ajili ya kufundisha wananchi namna ya kufuga samaki.   Akizungumza jana (17.03.2021) wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge, Kilimo, Mifugo na Maji ilipotembelea kituo cha ukuzaji viumbe maji kinachozalisha vifaranga vya samaki cha Kingolwira kilichopo Mkoani Morogoro, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amesema mkakati wa serikali kupitia vituo hivyo vitakavyokuwepo katika halshamauri zote za wilaya ni kuwa na samaki wengi wafugwao kwa njia mbalimbali ikiwemo ya mabwawa na kufikia uzalishaji wa samaki wa asilimia 50 kwa njia ya kufuga na asilimia 50 wanaotokana na maji ya asili.   “Kupitia tasnia hii ya ukuzaji viumbe maji tunataka kuweka nguvu kubwa ili tuweze kuvuna rasilimali ya uv...

WAFANYABIASHARA WAPEWA SIKU 5 KUONDOA MIFUGO KATIKA MNADA WA KIZOTA

Picha
Wafanyabiashara wa mifugo katika Mnada wa Kizota Jijini Dodoma wametakiwa kuacha kuhifadhi mifugo yao inayokwenda machinjioni katika eneo la mnada kwani kufanya hivyo ni kinyume na taratibu.   Agizo hilo limetolewa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul leo (16.03.2021) wakati alipotembelea mnada huo kwa lengo la kukagua shughuli zinazofanyika ambapo pia alikutana na baadhi ya wafanyabiashara wa mifugo.   Gekul amewaeleza wafanyabiashara hao kuwa zipo taratibu za uendeshaji wa Minada ya Upili ambapo mifugo ikishanunuliwa inatakiwa kuchukuliwa na sio kutuzwa hapo ikisubiri kupelekwa machinjioni.   “Hivyo natoa siku tano kwa wafanyabiashara wote ambao mnatunza mifugo yenu hapa mkisubiri kuipeleka machinjioni kuhakikisha mnaitoa na kuitafutia eneo jingine kwa ajili ya kuitunza,” alisema Naibu Waziri Gekul.   Aidha, Naibu Waziri Gekul aliwaeleza wafanyabiashara hao kuwa wizara imeshatenga fedha zaidi ya milioni 200 kwa ajili ya kuanza kuboresha...

WACHUNAJI NGOZI WASIOZINGATIA TARATIBU KUFUTIWA LESENI

Picha
Serikali imesema itawachukulia hatua kali ikiwemo kuwafutia leseni wachunaji wa ngozi katika machinjio ya Manispaa ya Morogoro wanaotoboa ngozi za mifugo na kuifanya kukosa thamani licha ya kupatiwa mafunzo na vitendea kazi.   Akizungumza (15.3.2021) mara baada ya kufanya ziara ya kukagua uzalishaji wa ngozi bora zinazohitajika katika soko, Kaimu Mkurugenzi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe, Bw. Gabriel Bura alisema licha ya kufanyika mafuzo ya uchunaji bora wa ngozi lakini bado wapo watu wanaokiuka taratibu zilizowekwa.   Alisema mafunzo yaliyotolewa yamesaidia kwa kiasi kikubwa upatikanaji wa ngozi bora lakini Serikali haitawafumbia macho baadhi ya wachunaji wa ngozi wanaoendelea kutoboa ngozi kutokana na mahitaji makubwa yaliyopo hasa katika viwanda vikubwa vya ngozi vilivyoanzishwa.   “Tulizitoa lesei hizi kwa sheria ya ngozi namba 18 ya mwaka 2008, lakini pia tulitoa mafunzo ya uchunaji wa ngozi ili kuzipa thamani ngozi mnazozalisha lakini k...

GEKUL AITAKA TALIRI KUJIENDESHA KIBIASHARA

Picha
Na. Elibariki Mafole, Mpwapwa   Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Pauline Gekul ameitaka Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) kujiendesha kibiashara ili iweze kukabiliana na changamoto zinazo ikabili.   Gekul ameyasema hayo leo (15.03.2021) wakati alipo tembelea kituo cha TALIRI na LITA Mpwapwa kwa lengo la kukagua kazi zinazofanywa na taasisi hizo.   Katika taarifa iliyosomwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu TALIRI, Dkt. Jonas Kizima ilielezea changamoto wanazokabiliana nazo zikiwemo za upungufu wa watumishi, uhaba wa vitendea kazi na uhaba wa rasilimali fedha kwa shughuli za kiutafiti. Lakini pia alizungumzia mikakati waliyonayo katika kukabiliana na changamoto hizo.   Kwa kuwa changamoto nyingi zinahitaji fedha ili kuzitatua ndipo Naibu Waziri Gekul akawaagiza TALIRI kujipanga vizuri ili sasa waweze kujiendesha kibiashara kwani kwa kufanya hivyo wataweza kutatua changamoto walizonazo badala ya kusubiri kupata fedha kutoka Serikalini.   Pi...

SOKO LA SAMAKI WAFUGWAO NA MAJI YA ASILI KUSHINDANISHWA

Picha
  Na. Edward Kondela   Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amesema serikali imeweka lengo la kuhakikisha Sekta ya Uvuvi kupitia ufugaji samaki inazalisha idadi kubwa ya samaki sambamba na samaki wapatikanao kwenye maji ya asili.   Akizungumza jana (10.03.2021) alipokuwa akikagua shughuli zinazofanywa na Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji cha Kingolwira kilichopo Mkoani Morogoro, Waziri Ndaki amesema tasnia ya ufugaji samaki imekuwa na mwitikio mkubwa kwa sasa kutokana na mahitaji ya soko la samaki kuongezeka hivyo jitihada nyingi zinafanyika kuongeza uzalishaji wa vifaranga vya samaki.   “Kwa sasa tasnia ya ufugaji samaki imekuwa ikitoa faida kubwa kwa wanaojishulisha na ufugaji hivyo natoa wito kwa watu kujitokeza kwa wingi kufuga samaki   na pia na toa wito kwa vituo vyetu vya ukuzaji viumbe maji vilivyopo nchini kuhakikisha vinaongeza uzalishaji wa samaki kwa kuwa mahitaji ya vifaranga ni mengi.” Amesema Mhe. Ndaki   Aidha, amesema W...

WAZIRI NDAKI ANUSA UBADHILIFU MNADA WA PUGU, AUONYA UONGOZI NA KUMUONDOA ASKARI KAZINI

Picha
Na. Edward Kondela Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amemtaka Mkuu wa Kikosi Maalum cha Kuzuia Wizi wa Mifugo (STPU) Kanda Maalum ya Dar es Salaam, kumuondoa kazini katika mnada wa Pugu, mkuu wa zamu na wenzake kwa tuhuma za kutoa taarifa zisizo sahihi za idadi ya mifugo inayoingia mnadani. Waziri Ndaki amesema hayo leo (10.03.2021) jijini Dar es Salaam, mara baada ya Waziri Ndaki kutembelea mnada wa Pugu ili kukagua namna watumishi wa umma wanaofanya kazi katika mnada huo wanavyohakikisha wanasimamia vyema mapato ya serikali. Mara baada ya kukagua vitabu vya taarifa za mifugo katika mnada huo, waziri huyo akabaini dosari katika taarifa za Kikosi Maalum cha Kuzuia Wizi wa Mifugo na kumtaka mkuu wa kikosi hicho Kanda Maalum ya Dar es Salaam Inspekta Nyangogo Justine kumuondoa katika mnada huo Sajenti Ahmad na wenzake waliokuwa zamu jana (09.03.2021) kwa tuhuma za kutoa taarifa zisizo sahihi za idadi ya mifugo inayoingia mnadani. Kufuatia hali hiyo Waziri Ndaki amemtaka Mkuu ...

TANGAZO

Picha
 

TAARIFA ZA UTEKELEZAJI MIFUGO, UVUVI ZATINGA BUNGENI

Picha
Wizara ya Mifugo na Uvuvi leo  imewasilisha taarifa zake za utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo kwa mwaka wa fedha uliopo (2020/2021) na mikakati iliyojiwekea katika utekelezaji wa miradi kwa mwaka ujao wa fedha (2021/2022) mbele ya kamati ya kudumu ya bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwenye moja ya kumbi za bunge jijini Dodoma.   Sekta ya Mifugo ndio ilikuwa ya kwanza kuwasilisha taarifa yake ambapo Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel alibainisha kuwa sekta yake iliidhinishiwa kiasi cha Shilingi bilioni 5 kwa mwaka wa fedha wa fedha uliopo likiwa ni ongezeko la takribani asilimia 60 ukilinganisha na mwaka wa fedha uliopita (2019/2020) ambapo sekta hiyo ilitengewa kiasi cha shilingi 3.   “Mhe. Mwenyekiti fedha hiyo ndo tumeitumia kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa majosho 20 yaliyojengwa katika Halmashauri mbalimbali za wilaya, kujenga kliniki na maabara 10 za mifugo ambazo zitaghar...