Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2019

TANZANIA YASHIRIKI KONGAMANO LA MATUMIZI ENDELEVU YA RASILIMALI ZA BAHARI NCHINI MSUMBIJI

Picha
Nchi zinazopakana na Bahari ya Hindi zikiwemo Tanzania, Kenya, Msumbiji na Afrika ya Kusini na Visiwa vya Ushelisheli zimepewa rai ya kuhakikisha zinafanya kila njia kulinda rasilimali za pamoja hususan zinazopakana na bahari ili ziweze kusaidia kukuza uchumi wa nchi hizo. Rai hiyo imetolewa na Rais wa Msumbiji Mhe. Filipe Jacinto Nyusi wakati wa ufunguzi wa kongamano la kujadili matumizi endelevu ya rasilimali za bahari linaloendelea katika mji wa Maputo nchini humo. Rais Nyusi amesema kongamano hilo la siku mbili lina umuhimu mkubwa kwa kuwa linafanyika wakati huu ambapo uvunaji holela na usiofuata utaratibu wa rasilimali za bahari umeshamiri katika nchi nyingi za bara la Afrika na Asia. Akihutubia washiriki wa Kongamano hilo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega ameelezea hatua mbalimbali ambazo nchi ya Tanzania imepiga katika kuhakikisha malengo ya milenia kuhusu uhifadhi na matumizi endelevu ya rasilimali za asili yanafikiwa. Mhe. Ulega amezita...

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI (MIFUGO) AAHIDI KUBORESHA WIZARA KUWA YA MFANO KIUTENDAJI SERIKALINI

Picha
                                                                                                                                                                  ...

SERIKALI ZA TANZANIA NA DENMARK ZAJA NA MPANGO WA KULINDA RASILIMALI ZA ZIWA TANGANYIKA.

Picha
SERIKALI ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Denmark kupitia Shirika la Misaada la Kimaendeleo (DANIDA) imesema kuna haja ya kuendeleza mapinduzi makubwa katika sekta ya uvuvi nchini ili kulinda rasilimali zipatikanazo katika maziwa, bahari na mito nchini. Akizungumza jijini Dodoma wakati wa kupokea taarifa ya utafiti uliofanywa katika Ziwa Tanganyika lililopo Mkoani Kigoma, kutazama mabadiliko ya tabia nchi katika eneo la ziwa hilo, Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega amesema utafiti huo umeonyesha wazi kuwa zipo athari zinazotokana na tabia nchi na sababu zingine kama idadi ya wavuvi kuongezeka na baadhi yao kutumia zana haramu za uvuvi na kuathiri mazingira ya ziwa na rasilimali zilizopo. Mhe. Ulega amesema mambo yote ambayo yamefanyiwa utafiti yakijadiliwa vyema litatolewa tamko la Sera ambayo itakuwa ni ushauri wa kitaalam ambao utaiongoza serikali ikiwa inaendelea kufanya maboresho ya kanuni na sheria za uvuvi. "Kitu hiki ni muhimu s...

WAFUGAJI KITETO WAKABIDHIWA HATI MILIKI YA NYANDA ZA MALISHO.

Picha
Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewezesha kupatiwa hati miliki ya kimila Nne (4) kwa kikundi cha wafugaji   cha Olengapa kupitia mradi wa Uendelezaji wa Nyanda za Malisho (SRMP). Tukio hilo la kukabidhi hati miliki ya kimila kwa Kikundi cha Wafugaji lilifanyika katika Kijiji cha Lengatei Wilaya ya Kiteto Mkoa wa Manyara. Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia mradi wa SRMP imeweza kutoa hati hiyo kwa kikundi cha wafugaji cha Olengapa vinavyoruhusu kutumia na kumiliki eneo la malisho kwa pamoja. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Sekta ya Mifugo,Prof Elisante Ole Gabriel, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Zakariyya Kera alisema, eneo hilo lililotengwa linaukubwa wa hekta 30,145. Alisema pia, lengo ni kuwapatia   haki wafugaji ya uhakika wa kumiliki Ardhi kwa shughuli zao za kiuchumu na kijamii. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Bw. Manyara Alexanda Mnyeti, Mku...

WAFUGAJI WAASWA KUBADILIKA KIFIKRA NA KUFUATA SHERIA

Picha
SERIKALI imewataka wafugaji nchini kubadili fikra zao na kutambua umuhimu wa kufuata sheria, taratibu na kanuni za nchi ili kujiepusha na mkono wa sheria pindi wanapoingiza mifugo yao katika hifadhi na mapori ya akiba. Akizungumza na baadhi ya wafugaji jana (20.04.2019) katika Wilaya ya Meatu, Mkoani Simiyu, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amesema baadhi ya wafugaji wamekuwa wakiingiza mifugo yao katika hifadhi na mapori ya akiba, hivyo kusababisha kutokuwepo kwa mahusiano mazuri kati yao na wahifadhi kwa madai ya kuonewa ilhali wahifadhi hao wanatakeleza sheria za nchi. “Tunatamani fikra za wafugaji wote nchini zibadilike na zianze kutambua umuhimu wa kufuata sheria, taratibu na kanuni, ndiyo msingi wa mafaniko. Niwaombe wafugaji wote nchini watambue kwamba Wizara ya Mifugo na Uvuvi itapenda wafugaji wafuate sheria, taratibu na kanuni, tukifanya hivyo tutakuwa marafiki wa wizara unapokuwa mhalifu unakuwa tena siyo mfugaji bali un...

NORWAY YAISAIDIA SEKTA YA UVUVI NCHINI

Picha
SERIKALI ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la NORAD, Norway imesaini mkataba wa uzalishaji samaki aina ya Sato zaidi ya tani 100,000 kwa mwaka katika kipindi cha miaka 10 ijayo. Akizungumza jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa mradi huo kwa niaba ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi,   mhe.Luhaga Joelson Mpina, Katibu Mkuu wa sekta ya Uvuvi   Dk. Rashid Tamatamah amesema,   mradi huo umekuja muda muafaka wakati nchi ina mahitaji makubwa. Amesema lengo la Serikali ni kuzalisha samaki kwa wingi ambapo utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano kwenye mabwawa. Amesema mradi huo umekuja kwa sababu ya kazi nzuri ya asasi ya Norges Vel, Chama cha Ukuzaji Viumbe Maji Tanzania (AAT) na Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA). Aliongeza kuwa katika kipindi cha miaka 20 sasa Tanzania imekuwa haifanyi vizuri katika sekta ya uvuvi ambapo imekuwa ikizalisha samaki tani 350,000 hadi 380,000 kwa mwaka."Samaki wanaozalishwa hivi sasa kwenye vy...