Nav bar

Jumatatu, 13 Mei 2019

WAFUGAJI KITETO WAKABIDHIWA HATI MILIKI YA NYANDA ZA MALISHO.




Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imewezesha kupatiwa hati miliki ya kimila Nne (4) kwa kikundi cha wafugaji  cha Olengapa kupitia mradi wa Uendelezaji wa Nyanda za Malisho (SRMP).

Tukio hilo la kukabidhi hati miliki ya kimila kwa Kikundi cha Wafugaji lilifanyika katika Kijiji cha Lengatei Wilaya ya Kiteto Mkoa wa Manyara.

Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia mradi wa SRMP imeweza kutoa hati hiyo kwa kikundi cha wafugaji cha Olengapa vinavyoruhusu kutumia na kumiliki eneo la malisho kwa pamoja.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Sekta ya Mifugo,Prof Elisante Ole Gabriel, Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu Bw. Zakariyya Kera alisema, eneo hilo lililotengwa linaukubwa wa hekta 30,145.

Alisema pia, lengo ni kuwapatia  haki wafugaji ya uhakika wa kumiliki Ardhi kwa shughuli zao za kiuchumu na kijamii.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Bw. Manyara Alexanda Mnyeti, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Bw. Tumaini Magesa alisema, nashukuru wizara ya Mifugo na uvuvi kuheshimu ilani ya Chama cha mapinduzi kwasabau ni hitaji la chama tawala na hili limefanikiwa.




Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu Bw. Zakariyya Kera akisoma hotuba kwa ufupi kwa niaba ya Katibu  Mkuu sekta ya Mifugo.



Mwenyekiti wa kikundi cha Olengapa Bw. Kilekeni Noongejeck akipokea hati miliki ya kimila kwa niaba ya kikundi kutoka kwa mgeni rasmi  Bw. Tumaini Magesa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni