Nav bar

Jumatatu, 29 Oktoba 2018

UZINDUZI WA BODI YA KAMPUNI YA RANCHI ZA TAIFA (NARCO)*



Bodi ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) imezinduliwa rasmi  tarehe 27/10/2018 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Joelson Mpina.

Ninawashukuru wote kwa kukubali uteuzi huu kwa sababu natambua hakuna kazi iliyo nyepesi - Waziri Mpina

Namshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uteuzi huu kwani ametambua uwezo na uzalendo wenu, Nchi hii inapaswa kuendelezwa na wananchi wazalendo watakaowezesha Nchi kusonga mbele - Mhe. Mpina

Ni matarajio yangu kuwa; Bodi hii itaweza kufikia Mikakati tuliojiwekea na ndani ya Wiki mbili zijazo lazima kikao cha Bodi kiitishwe ili kuanza utekelezaji wa mikakati tutakayojiwekea - Waziri Mpina

Sekta ya Mifugo ina mchango mkubwa katika ujenzi wa taifa letu ambapo mpaka sasa jumla ya Mifugo tuliyonayo ni mil 57 na tunazalisha Lita Bil 2.4 za Maziwa - Waziri Mpina.

Tunahitaji mpaka mwakani tuongeze idadi kubwa ya Mifugo kwa sasa, tuna Ngombe milioni 30.5, mbuzi 18.8 mil, kondoo Mil. 5.3, nguruwe Mil. 1.9, Kuku wa kienyeji Mil. 38.2, na wa kisasa ni Mil. 36.6.

Mpaka sasa idadi ya mifugo inayouzwa Nje ya Nchi kwa njia haramu na halali ni asilimia 70 na mifugo michache tuliobaki nayo ni asilimia 30 - Waziri Mpina.

 Mazao mengi yanaingia Nchini bila kufuata taratibu na Mifugo inatoroshwa kwakuwa hatuna Viwanda vya uhakika hapa Nchini, tuna viwanda 32 lakini ni machinjio- Waziri Mpina.

Ifike mahali kwenye Taasisi za Serikali ikiwemo na NARCO Kuwe na viwanda vya uhakika Itakuwa ni mfano na kielelezo kwa Sekta binafsi - Waziri Mpina.

 Tumepandisha tozo kuanzia 1000 hadi 10,000 ili kila mmoja aweze kumiliki eneo ambalo anauwezo
nalo - Waziri Mpina.

Shirika lifike mahali linatoa nyama ya ng’ombe ndani na Nje ya Nchi na kutengenza bidhaa zitokananzo na ngozi - Waziri Mpina

Naitaka Bodi na timu nzima  kuhakikisha mnaandaa mpango kazi na wa biashara kwa kushirikiana
na Dawati la Sekta Binafsi - Waziri Mpina

 kwa mashirika yangu yote kabla ya tarehe 30/11/2018 lazima tuandae gawio letu kwa Serikali - Waziri Mpina

Ni lazima kila mmoja afahamu wajibu wake ili tuweze kufikia mafanikio tuliyojipangia - Waziri Mpina

Watendaji wa Wizara yangu mtakuwa na kazi ya kusimamia mikakati tuliojiwekea inatekelezaa hadi
kufikia tarehe 30/11/2018 nipatiwe mikakati hiyo - Waziri Mpina.

Naimani pamoja na magumu haya mageuzi lazima yafanyike “ penye nia Pana njia” - Waziri Mpina.

Bodi inayozinduliwa leo iko kisheria kwa mujibu wa Mashirika ya Umma na. 2 ya mwaka 1992 kifungu cha 9 (1). Natangaza rasmi uzinduzi wa Bodi hii - Waziri Mpina.

 Naamini kuzinduliwa kwa Bodi hii kutaleta mapinduzi Makubwa na ni matumaini tutalinda rasilimali za Nchi yetu - KM Prof Ole Gabriel.

Bodi hii imesheheni wataalam wanaoaminika,tunaamini wataenda kuondoa changamoto mbalimbali
zinazolikabili shirika hili - Katibu Mkuu, Prof Ole Gabriel.

Tanzania ni Nchi ya 2 kuwa na ng’ombe wengi lakini hatufanyi vizuri kwenye eneo hili ila naimani
wajumbe hawa watafanya kazi ambayo wameiandaa kuifanya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge Kilimo, Mifugo, na Maji, Mhe. M. Mgimwa.

 Tunataka mwakani tuwe na idadi kubwa ya ng’ombe ambapo tukijidhatiti kukuza Ranchi zetu na
kuhusisha Sekta binafsi tunauwezo wa kupata wadau nje na ndani ya Nchi. - Mhe M. Mgimwa .

Namshkuru Rais Dkt. Magufuli kwa uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi hii, kwani najua umezingatia mengi pamoja na utendaji wako wa kazi na uzoefu wa kuitumikia nchi ya Tanzania pia tunaamini ni chaguo sahihi kwa wakati sahihi - Katibu Mkuu Mifugo Prof. Ole Gabriel.

Namshukuru Mhe. Rais kwa kuniteua naahidi mimi na wajumbe tuna uwezo wa kuifanya kazi hii -
Mwenyekiti wa Bw. Bodi Paul Kimiti.

Tutajenga timu ya kufanya kazi kwani uzoefu uliopo katika vichwa vya wajumbe hawa utakua ni
rasilimali ya kubwa katika utendaji wetu - Mwenyekiti wa Bodi Bw. Paul Kimiti

Tayari tumeanza kuweka malengo na mikakati ya utendaji kazi itakayorudisha imani ya shirika la
NARCO - Mwenyekiti wa Bodi Bw. Paul Kimiti.




Mhe Waziri akimpongeza  Mwenyekiti wa Bodi ya NARCO Bw. Paul Kimiti baada ya kuteuliwa na Mhe. Raisi.

Mhe. Waziri akisalimiana na Katibu Mkuu Mifugo

Picha ya pamoja Mhe. Waziri akiwa na Bodi ya NARCO iliyoteuliwa, Waheshimiwa Wabunge, Wakurugenzi na Watumishi wa Baraza wakati wa uzinduzi wa Bodi , Jijini Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni