Nav bar

Alhamisi, 21 Desemba 2017

ZIARA YA KATIBU MKUU SEKTA YA MIFUGO DKT. MARIA MASHINGO ALIPOTEMBELEA MKOA WA KAGERA

Katibu Mkuu waWizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Mary Mashingo akiongea na wafugaji wa nchini Uganda katika eneo la Omwaarogwamabaare akiwa na balozi wa Uganda nchini Tanzania Mhe. Richard Tumusiime Kabonero waliomzunguka ni wataalam mbalimbali kutoka Wizarani.

Katibu Mkuu waWizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Mary Mashingo(aliyeshikafimbo) akipima kina cha Kisima kilitengenezwa kienyeji kwaajili ya kunyweshea mifugo katika eneo la Kafunjo Wilaya ya Missenyi Mkoani Kagera. Waliomzunguka ni wataalam mbalimbali kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizaraya Mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa na Halmashauri ya Missenyi.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Mifugo, Dkt. Mary Mashingo (aliyenyanyuamkono) akimweleza jambo Balozi wa Uganda nchini Tanzania Mhe. Richard Tumusiime Kabonero walipokuwa katika ziara ya kikazileo kwenye Mto Kagera katikakijiji cha Kakunyu Wengine kushoto kwa Katibu Mkuu ni Dkt. Martin  Ruheta Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kulia kwa Balozi ni Suleiman Ahmed saleh, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni