Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatarajia kuanza kutumia mfumo wa usimamizi wa utoaji vibali mbalimbali vya kusafirisha mifugo na mazao yake ndani na nje ya nchi unaojulikana kama “ Mifugo Management Information System (MIMIS)” ambao unalenga kuboresha mazingira ya ufanyaji wa biashara za Mifugo, kukata na kuhuisha leseni za wataalam wa Mifugo na vibali vinavyohusu uingizaji, uzalishaji na uuzaji wa vyakula vya samaki. Hayo yamebainishwa leo na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Mifugo Dkt. Charles Mhina alipokuwa akifungua mafunzo ya matumizi ya mfumo huo kwa wadau na wataalam kutoka sekta za Mifugo na Uvuvi yaliyofanyika leo (18.05.2022) kwenye hoteli ya Royal Village jijini Dodoma. “Uwepo wa mfumo huu utatusaidia kuokoa muda wa kushughulikia vibali lakini pia utaongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuokoa fedha za Serikali kwa sababu “Control Number” itazalishwa pale mtu anapofanya maombi tofauti na sasa ambapo mtu a...
Na. Daudi Nyingo – Iringa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede, ameongoza zoezi la utambuzi na uchanjaji wa mifugo mkoani Iringa, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Utoaji Chanjo na Utambuzi wa Mifugo iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa mkoani Simiyu hivi karibuni. Akizungumza Julai 3, 2025, mkoani Iringa, Dkt. Mhede alisema kuwa kampeni hiyo ya miaka mitano inalenga kuchanja mifugo yote nchini kama sehemu ya uwekezaji katika sekta ya mifugo, unaowaletea faida wafugaji na kukuza uchumi wa taifa. “Tunalenga kuchanja ng’ombe wapatao 400,000 hapa Iringa. Tayari tumejiridhisha kuwa chanjo zipo za kutosha, na tumeanza kutembelea maeneo mbalimbali kama Kalenga na shamba la mifugo la Kibete, linalomilikiwa na Richard Philips, kuhakikisha zoezi linaenda vizuri,” alisema Dkt. Mhede. Mbali na ng’ombe, Dkt. Mhede alibainisha kuwa chanjo pia zitatolewa kwa kuku, na aliwahimiza wananchi ...
Na. Edward Kondela Serikali imesema itahakikisha inachukua hatua ya kuwepo kwa taratibu maalum zilizo wazi kwenye biashara ya mabondo ya samaki ili kujiridhisha upatikanaji wake hadi kufika viwandani kwa ajili ya kuchakatwa. Akizungumza (05.03.2024) jijini Mwanza na wamiliki wa viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi katika jiji hilo, wakati akimwakilisha Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe, Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi Prof. Mohammed Sheikh amesema serikali itahakikisha inaweka utaratibu ili kujiridhisha namna ya upatikanaji wa mabondo. Prof. Sheikh amebainisha hayo baada ya baadhi ya wamiliki wa viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi kulalamika kuwa baadhi ya wavuvi wamekuwa wakivua samaki ambao wako chini ya viwango vinavyotakiwa viwandani wakiwa na lengo la kuuza mabondo kwenye viwanda vya kuchakata mabondo hayo na kuharibu mazalia ya samaki. Ameongeza kuwa lazima kuwepo utaratibu maalum kujua upatikanaji wa mabondo hadi kufika kwenye viwanda kwa ajili uchaka...
Maoni
Chapisha Maoni