Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi inatarajia kuanza kutumia mfumo wa usimamizi wa utoaji vibali mbalimbali vya kusafirisha mifugo na mazao yake ndani na nje ya nchi unaojulikana kama “ Mifugo Management Information System (MIMIS)” ambao unalenga kuboresha mazingira ya ufanyaji wa biashara za Mifugo, kukata na kuhuisha leseni za wataalam wa Mifugo na vibali vinavyohusu uingizaji, uzalishaji na uuzaji wa vyakula vya samaki. Hayo yamebainishwa leo na Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia sekta ya Mifugo Dkt. Charles Mhina alipokuwa akifungua mafunzo ya matumizi ya mfumo huo kwa wadau na wataalam kutoka sekta za Mifugo na Uvuvi yaliyofanyika leo (18.05.2022) kwenye hoteli ya Royal Village jijini Dodoma. “Uwepo wa mfumo huu utatusaidia kuokoa muda wa kushughulikia vibali lakini pia utaongeza kasi ya ukusanyaji wa mapato ya Serikali na kuokoa fedha za Serikali kwa sababu “Control Number” itazalishwa pale mtu anapofanya maombi tofauti na sasa ambapo mtu a...
Na. Daudi Nyingo – Iringa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede, ameongoza zoezi la utambuzi na uchanjaji wa mifugo mkoani Iringa, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Utoaji Chanjo na Utambuzi wa Mifugo iliyozinduliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, alipokuwa mkoani Simiyu hivi karibuni. Akizungumza Julai 3, 2025, mkoani Iringa, Dkt. Mhede alisema kuwa kampeni hiyo ya miaka mitano inalenga kuchanja mifugo yote nchini kama sehemu ya uwekezaji katika sekta ya mifugo, unaowaletea faida wafugaji na kukuza uchumi wa taifa. “Tunalenga kuchanja ng’ombe wapatao 400,000 hapa Iringa. Tayari tumejiridhisha kuwa chanjo zipo za kutosha, na tumeanza kutembelea maeneo mbalimbali kama Kalenga na shamba la mifugo la Kibete, linalomilikiwa na Richard Philips, kuhakikisha zoezi linaenda vizuri,” alisema Dkt. Mhede. Mbali na ng’ombe, Dkt. Mhede alibainisha kuwa chanjo pia zitatolewa kwa kuku, na aliwahimiza wananchi ...
Na. Stanley Brayton, WMUV - Dodoma ◼️Waelezewa athari za kulisha Mifugo katika maeneo ya Hifadhi za Misitu. Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, amewataka wafugaji Wilayani Bahi na Chamwino kupanda Malisho kwa ajili ya Mifugo ili kuepukana na changamoto za kukosa Malisho ya Mifugo. Akizungumza katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika leo Aprili 15, 2025, Mkoani Dodoma, katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Wilaya ni Bahi, Ndg. Mhinte, amesema yapo maeneo muhimu ya Malisho ambayo yametengwa na Serikali ili kutatua changamoto za Malisho. "yapo maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya Malisho japo yanapungua kadri Mifugo inavyozidi kuongezeka, na ni muhimu kuhakikisha kila mfugaji anapanda Malisho kwa ajili ya Mifugo yake" amesema Ndg. Mhite Vilevile, Ndg. Mhite amebainisha kuwa maeneo ya Malisho yanapungua kadri Mifugo na watu wanavyoongezeka, kiasi cha kwamba kun...
Maoni
Chapisha Maoni