WANUFAIKA WA TASFAM MTAMA WAHIMIZWA KUTUMIA KANUNI BORA ZA UKUZAJI VIUMBE MAJI

Na. Martha Mbena. 

Wanufaika wa Mradi wa kuendeleza na kusimamia Uvuvi wa Baharini na Ukuzaji Viumbe Maji (TASFAM) wa Wilaya ya Mtama mkoani Lindi wamehimizwa kutumia kanuni bora za Ukuzaji Viumbe maji.

Akizungumza wakati wa kutoa Elimu kuhusu kanuni ya Viumbe maji Machi 28,2026, Afisa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Justine Ndayeze, amewasisitiza wanufaika hao wasifanye shughuli pasipo kufuata kanuni bora, sheria na taratibu za Ukuzaji viumbe maji ili kuweza kufanya shughuli hizo kwa Uhuru bila kuvunja sheria.

"Tusifanye shughuli kimya kimya bila kufanya taratibu zote zilizowekwa na Wizara za Ufugaji na Ukuzaji viumbe maji", Amesema  Bw. Ndayeze.

Aidha, Ndayeze ameongeza kusema kuwa kanuni inasisitiza kufuata kanuni kwa kufuata taratibu zote za kutunza mazingira ya viumbe maji, kupata mbegu bora, kukata vibali vya kusafirisha mazao ya uvuvi na kuwa na kumbukumbu za shughuli za ufugaji.

Kwa upande wake Mnufaika wa mafunzo hayo Bw. Hassan Namkanda wa kata ya Shuka, Wilaya ya Mtama, Mkoani Lindi ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuwaletea mafunzo ya ufugaji Ukuzaji viumbe maji na elimu ya kanuni bora kwa Wilaya ya Mtama kwani wanaahidi kufuata sheria na kanuni zote zilizowekwa na Wizara hiyo.

Afisa Uvuvi Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Happy Kapinga akiotoa elimu ya kuongeza mnyororo wa thamani wa zao la mwani wakati wa mafunzo kwa Wakulima wa Mwani na wafugaji wa  Jongoo Bahari  yaliyotolewa kupitia mradi wa TASFAM Machi 28, 2026, Wilaya ya Mtama, Mkoani Lindi.

Mnufaika wa mafunzo ya kuwajengea uelewa Wakulima wa zao la mwani na kanuni za Ufugaji viumbe maji kutoka kata ya Shuka,  Mkoani Lindi Bw. Hassani Namkanda (aliyesimama) akielezea namna ambayo wanafanya ukulima wa mwani na changamoto wanazopitia wakati mafunzo hayo yanaendelea yanayotolewa na Mradi wa TASFAM wilayani humo, Machi 28,2026.

Afisa uvuvi wa kituo cha Ukuzaji viumbe maji kanda ya Kusini Nyengedi, mkoa wa Lindi Bw. Festo Joseph (aliyesimama) akitoa elimu ya ufugaji jongoo Bahari kwa wanufaika wa mafunzo yanayotolewa na mradi wa TASFAM wa Wilaya ya Mtama, Mkoani Lindi, Machi 28,2026.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO