SERIKALI YAONGEZA NGUVU KWA MAAFISA UGANI

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kuimarisha uwezo wa maafisa ugani wa sekta ya mifugo kwa kuwapatia mafunzo rejea yanayolenga kuboresha utoaji wa huduma kwa wafugaji na kuongeza uzalishaji wa mifugo nchini.

Mafunzo hayo yaliyodumu kwa siku mbili  Kwa upande wa maafisa ugani wa Mifugo yamehitimishwa leo Machi 10, 2026 Katika ukumbi wa IFM  Wilayani Chato mkoani Geita kwa kuwahusisha maafisa ugani kutoka Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi.

Akizungumza wakati wa hitimisho la mafunzo hayo, Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambaye pia ni Afisa Mifugo Mkuu, Bi. Mary Yongolo amewashukuru maafisa ugani kwa nidhamu waliyoionesha katika kipindi chote cha mafunzo hayo.

"Hakikisheni maarifa mliyoyapata yawe chachu ya kuboresha utendaji kazi wenu pindi mrejeapo vituoni ili kuleta tija katika sekta ya mifugo." Amesema Bi. Yongolo

Kwa upande wake, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Dkt. Sostenes Nkombe, amewapongeza washiriki kwa ushiriki wao katika mafunzo hayo na kuwataka kuwa mfano kwa maafisa wengine watakaporejea katika vituo vyao vya kazi.

Aidha, amesema kuwa mafunzo hayo yana mchango mkubwa katika kuimarisha ufanisi wa maafisa ugani katika kuwahudumia wafugaji na kusaidia maendeleo ya sekta ya mifugo katika ngazi za halmashauri.

Kwa upande wake mwakilishi wa washiriki wa mafunzo hayo, Frank Ipugute ambaye ni Afisa Mifugo Halmashauri ya Wilaya ya Chato, ameishukuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuandaa mafunzo hayo na kuomba yaendelee kutolewa mara kwa mara, pia yatolewe katika ngazi za Halmashauri ili yaweze kuwafikia maafisa ugani wengi zaidi na kuboresha huduma kwa wafugaji.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Ndg. Mary Yongolo Afisa Mifugo Mkuu, akitoa neno la Shukrani Kwa  Maafisa Ugani wa Mifugo Kwa nidhamu waliyooshesha wakati wa mafunzo  yaliyojumuisha  Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi yaliyofanyika katika Ukumbi IFM, Machi 10, 2026 Chato Mkoani Geita.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Dkt. Sostenes Nkombe, akizungumza wakati wa mafunzo rejea kwa maafisa ugani wa sekta ya mifugo, ambapo amewapongeza washiriki kwa ushiriki wao na kuwataka kuwa sehemu ya mfano Kwa maafisa wengine pindi warudipo vituoni, mafunzo hayo  yamefanyika katika Ukumbi wa IFM Chato, Machi 10, 2026 Mkoani Geita.

Afisa Mifugo Mwandamizi, Ahmed Mziray kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi akitoa wasilisho la rasimu ya mbari  kwa ajili yakupata maoni ya wadau wakati wa mafunzo rejea kwa maafisa ugani wa sekta za mifugo na uvuvi wa Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi kwenye ukumbi wa IFM Chato mkoani Geita, Machi 10, 2026

Afisa TEHAMA kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Ndg. Stanislaus Chayeka akitoa wasilisho juu ya Mfumo wa MIMIS, jinsi yakusaidia wadau kujisajili kwenye mfumo kuomba vibali na kusajili huduma mbalimbali na jinsi ya kuwasaidia wadau kutumia mfumo huo, kwenye mafunzo rejea kwa maafisa ugani wa sekta za mifugo na uvuvi Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi kwenye ukumbi wa IFM Chato mkoani Geita, Machi 10, 2026

Picha ni maafisa ugani wa mifugo wakiwa kwenye mafunzo rejea Kwa Katika Sekta ya Mifugo kwa Kanda ya Ziwa na Kanda ya Magharibi, yanayoendelea kufanyika katika ukumbi wa IFM, Machi 10, 2026 Chato mkoani Geita.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO