MHE. KAMANI AITAKA FETA KUONGEZA UZALISHAJI WA VIFARANGA VYA SAMAKI

Na. Stanley Brayton, WMUV

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng’wasi Damas Kamani, ameitaka Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) kuongeza uzalishaji wa vifaranga vya samaki kutoka kiwango cha sasa na kufikia kati ya milioni 5 hadi 10 kwa mwezi, ili kuchochea ukuaji wa Sekta ya uvuvi na kuongeza tija kwa wananchi.

Akizungumza leo Machi 5, 2026 jijini Dodoma katika hafla ya uzinduzi wa Bodi ya Tatu ya Ushauri ya FETA, Mhe. Kamani amesema kuwa ongezeko la uzalishaji wa vifaranga litasaidia kuimarisha shughuli za ukuzaji viumbemaji na kuongeza mchango wa Sekta ya uvuvi katika Pato la Taifa.

"Bodi mpya inapaswa kusimamia kwa karibu Mpango Mkakati wa Wakala, na kuhakikisha upatikanaji wa mbegu bora za samaki, pamoja na kushirikiana na Taasisi nyingine zikiwemo Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), katika kuanzisha Mpango wa Kitaifa wa kuboresha mbegu za mazao ya viumbe 

maji" amesema Mhe. Kamani.

Aidha, Mhe. Kamani amewataka wajumbe wa Bodi hiyo kuimarisha mafunzo ya vitendo kwa vijana kupitia programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (BBT - Uvuvi) ili kuwawezesha kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika uchumi wa Buluu.

Katika hafla hiyo, Mhe. Kamani amezindua rasmi Bodi ya Tatu ya Ushauri ya FETA na kusisitiza kuwa Serikali chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, itaendelea kuiwezesha sekta ya uvuvi kwa maendeleo endelevu ya Taifa.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agness Meena amesema ili kuendeleza tasnia hiyo ya Uvuvi kwa njia endelevu, Wizara inahitaji wataalamu wenye ujuzi stahiki, ambao wanapatikana kupitia FETA. 

Vilevile Bi. Meena amempongeza mwenyekiti na wajumbe wote wa Bodi Kwa kuteuliwa, na kuwapongeza Kwa dhumuni la kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Naye, Mwenyekiti wa Bodi ya Tatu ya Ushauri ya FETA, Dkt. Blandina Lugendo amesema malengo ya FETA yatatekelezwa kikamilifu na weledi,  na pia ameiomba Wizara iweze kuwajengea miundombinu mipya ya kuweza kuendesha Taasisi hiyo.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) Dkt. Semvua Isa Mzighani amesema jukumu kuu la FETA ni kutoa elimu juu Ukuzaji Viumbe maji, pia wamepewa jukumu la kuboresha miundombinu ya Kampasi za Uvuvi ili kutoa wataalamu watakaosimamia bandari za uvuvi na kuanzisha kozi ya kimataifa ya uangalizi wa bandari.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Kamani (kushoto), akimkabidhi Mwenyekiti wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), Dkt. Blandina Lugendo (kulia), Muongozo wa Malengo ya Taasisi hiyo, katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya FETA, iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Kamani, akihutubia Watendaji Wakuu wa Wizara pamoja na Wajumbe wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya FETA, iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Agnes Kisaka Meena, akizungumza na Watendaji Wakuu wa Wizara pamoja na Wajumbe wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya FETA, iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Mwenyekiti wa Bodi ya Tatu ya Ushauri ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), Dkt. Blandina Lugendo, akizungumza na Watendaji Wakuu wa Wizara pamoja na Wajumbe wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya FETA, katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), Dkt. Semvua Isa Mzighani, akizungumza na Watendaji Wakuu wa Wizara pamoja na Wajumbe wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya FETA, katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi hiyo, iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Picha ni Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Wajumbe wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), wakimsikiliza Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Kamani (hayupo pichani), katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya FETA, iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Ng'wasi Kamani (katikati waliokaa), akiwa kwenye picha ya pamoja na Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, katika Hafla ya Uzinduzi wa Bodi ya tatu ya Ushauri ya Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), iliyofanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Gerwill, Machi 5, 2026 Dodoma.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO