KINGOLWIRA INAFAA KUWA KITUO KIKUBWA CHA UKUZAJI VIUMBEMAJI NCHINI - PROF. SHEIKH
Na. Stanley Brayton
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Prof. Mohammed Ali Sheikh amesema Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kinafaa kuwa Kituo kikubwa na cha Kitaifa cha Ukuzaji Viumbemaji nchini kwani kina Miundombinu nyinyi ambaazo zinajengwa na za kisasa.
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, alipotembelea Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kwa ajili ya kukagua Miundombinu na Uzalishaji, leo Machi 2, 2026 Mkoani Morogoro, Prof. Sheikh amesema Kituo kinazalisha vifaranga 600,000 kwa mwaka ikiwa kuna Vizimba 6 tu.
"kwa hiyo ni vyema kuharakisha kujenga Miundombinu nyingine haraka hili kuweza kuzalisha vifaranga vya Samaki zaidi ili wananchi wape kufuga.” amesema Prof. Sheikh
Aidha, Prof. Sheikh amesema Mradi huo wa Ukuzaji Viumbemaji wa Kingolwira unaendelea kuboreshwa zaidi kwa kutengeneza Vizimba vingine na Miundombinu nyingine ambazo zitakuwa zinazalisha vifaranga kwa wingi.
Vilevile, Prof. Sheikh amewataka Wataalam wa Kituo cha Ukuzaji Viumbemaji cha Kingolwira kufanya kazi kwa bidii na kuhakikisha vifaranga wanapatika kwa wingi na wenye ubora.





Maoni
Chapisha Maoni