KAMATI YA BUNGE YAPONGEZA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA TAFICO, CHANJO YA MIFUGO

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeipongeza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kutekeleza miradi ya maendeleo inayolenga kuongeza uzalishaji na mchango katika pato la taifa.

Mwenyeketi wa Kamati hiyo Mhe. Deoudatus Mwanyika ametoa pongezi hizo leo Machi 10, 2026 Bungeni Dodoma kwa niaba ya wajumbe baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) na Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa mifugo ilizinduliwa Juni 2025.

“Kama kamati tunaipongeza wizara kwa kuelimisha wafugaji na jamii kwa ujumla kuhusu chanjo, zoezi hili lilikuwa na mvutano sana kutokana na ukosefu wa elimu lakini sisi kamati tulisema ni lazima chanjo ifanyike. lakini pia, tunapongeza kwa miradi ya meli za TAFICO kwa ajili ya uvuvi wa Bahari Kuu, kamati hii imelipigania sana suala hili” alisema Mhe. Mwanyika.

Awali akitoa taarifa ya miradi inayotekelezwa na TAFICO Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo CPA Shaibu Matessa amesema jumla ya ajira za moja kwa moja elfu 13,049 zitazalishwa kutokana na miradi inayoendeshwa na TAFICO ambapo hadi sasa shirika hilo limenunu meli mbili za uvuvi wa Bahari Kuu kati ya meli tano zinazopangwa kununuliwa.

Kuhusu Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Benezeth Lutege amesema hadi kufikia Februri 2026 jumla ya mifugo  50, 215, 441 sawa na asilimia 65. 8 ya kuchanja mifugo 76, 323, 300 huku mifugo 2, 590,200 ikitambuliwa sawa na asilimia 15 ya lengo la kutambua mifugo 17,224,200 nchi nzima.

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deudatus Mwanyika akizungumza  wakati wa kikao cha kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi ya Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) na Kampeni ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo, kilichofanyika leo Machi 10, 2026 Bungeni Jijini Dodoma.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Uvuvi Tanzania (TAFICO) CPA Shaibu Matessa akiwasilisha utekelezaji wa miradi ya shirika hilo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo leo Machi 10, 2026 Bungeni Dodoma.

Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Dkt. Benezeth Lutege akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo na Utambuzi wa Mifugo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda,Biashara,Kilimo na Mifugo leo Machi 10, 2026 Bungeni Dodoma.

Mwenyekiti wa Kamati ya  Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo Mhe. Deudatus Mwanyika akiongoza kikao hicho, leo Machi 10, 2026

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally ( watatu kulia) akiwa pamoja na watendaji wa wizara kusikiliza hoja za Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo wakati wa kikao kilichofanyika leo Machi 10, 2026 Bungeni Jijini Dodoma.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO