TPHPA KUIMARISHA MAHUSIANO NA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA) waazimia kuimarisha mahusiano ya kiutendaji kazi katika utumiaji wa teknolojia inayoweza kutambua vinasaba vya virus, bakiteria, fangasi, na vimelea wengine wa magonjwa ya wanyama na mimea (NANOPODS) na matumizi ya ndege nyuki ya ufuatiliaji wa magonjwa.

Akizungumza, Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Nchini, Dkt. Benezeth Lutege leo Februari 06, 2026 mara baada ya kutembelea Makao Makuu ya Ofisi ya TPHPA iliyopo Mkoani Arusha, amesema wamejadiliana juu ya matumizi ya teknolojia ya kisasa ya ufuatiliaji wa magonjwa ya mifugo na mimea, inayotumika katika mashamba ya parachichi, na kutumika katika ufuatiliaji wa magonjwa ya mifugo.

Aidha, Dkt. Lutege amebainisha wazi kuwa mazungumzo hayo yalikuwa na lengo la kujifunza namna taasisi hiyo ilivyofanikiwa katika kufungua Masoko 408 ya kimataifa ya mazao ya kilimo ndani ya miaka 2.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Prof. Joseph Ndunguru ameonesha nia ya kuandaa Hati ya Maelewano (MoU) kati ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Taasisi ya TPHPA ili kuimarisha mahusiano katika maeneo ya; mafunzo ya matumizi ya teknolojia ya nanopods na matumizi ya ndege nyuki katika ufuatiliaji wa magonjwa, ufuatiliaji wa pamoja, mikataba ya masoko na eneo la utambuzi na utafiti.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru (katikati), akizungumza na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Nchini, Dkt. Benezeth Lutege (wa kwanza kulia), kuhusu kuimarisha mahusiano kati ya Taasisi hizo mbili katika utumizi wa Teknolojia ya Utambuzi wa vinasaba vya virusi, bakiteria, fangasi na vimelea wengine wa magonjwa ya wanyama na mimea, mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Makao Makuu ya TPHPA, Februari 06, 2026, Arusha

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania (TPHPA), Prof. Joseph Ndunguru (mstari wa mbele katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watendaji wa Serikali, mara baada ya kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Huduma za Mifugo Nchini, Dkt. Benezeth Lutege (wa pili kulia mstari wa mbele), kuhusu kuimarisha mahusiano kati ya Taasisi hizo mbili katika utumizi wa Teknolojia ya Utambuzi wa vinasaba vya virusi, bakiteria, fangasi na vimelea wengine wa magonjwa ya wanyama na mimea, mazungumzo yaliyofanyika katika Ofisi ya Makao Makuu ya TPHPA, Februari 06, 2026, Arusha

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO