NARCO YATAKIWA KUONGEZA UZALISHAJI MAZAO YA MIFUGO

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede ameisisitza  Kampuni ya Ranchi za Taifa  Nchini (NARCO) kutekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wakati wa ufunguzi wa Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na maelekezo ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally, ya kuleta ufanisi wa Kampuni hiyo na kuzalisha mazao yenye ubora katika sekta ya mifugo hapa nchini.

Dkt. Mhede ametoa rai hiyo leo Februari 05, 2026 Makao Makuu ya NARCO mjini Dodoma wakati wa kikao kazi cha utekelezaji wa maelekezo ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi kuhusu utekelezaji wa maagizo ya Rais ya kuongeza ufanisi wa Kampuni hiyo katika  kufanya mageuzi ya sekta ya mifugo. 

“Kampuni hii inatakiwa iongoze kwa kuzalisha mazao ya mifugo yenye ubora, niwasihi tujitoe kwa nguvu zote katika kutekeleza maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan  pamoja na maelekezo ya Waziri wetu, Mhe. Balozi Dkt. Bashiru Ally” alisema Dkt. Mhede.

Aidha, ameitaka NARCO kushirikiana na Bodi ya Nyama Tanzania katika kusimamia ufanisi wa machinjio  kuwa bora, kuongeza upatikanaji wa soko  la biashara ya nyama ndani na nje ya nchi.

Vile vile Dkt. Mhede aliwahimiza watendaji wa NARCO kuongeza kasi katika kutekeleza majukumu yao kwa kuzingitia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2050.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede akizungumza wakati wa kikao kazi kilichofanyika leo Februari 5, 2026, Makao Makuu ya NARCO Dodoma Mjini.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Edwin Mhede akiongoza kikao kazi cha kutekeleza  maagizo ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu ufanisi wa NARCO, kilichofanyika leo Februari 5, 2026, Makao Makuu ya NARCO Dodoma Mjini.

Wataalam wa Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO) wakimsikiliza Dkt. Edwin Mhede (hayupo, pichani) wakati wa  kikao kazi cha utekelezaji wa maagizo ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu ufanisi wa NARCO, kilichofanyika leo Februari 5, 2026, Makao Makuu ya NARCO yaliyopo Dodoma Mjini.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhede (watano kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na wataalam wa Kampuni ya Ranchi ya Taifa (NARCO) baada ya kufanya  kikao cha utekelezaji wa maagizo ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhusu ufanisi wa NARCO, kilichofanyika leo Februari 5, 2026, Makao Makuu ya NARCO Dodoma Mjini.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

LESENI, VIBALI VYA MAZAO YA MIFUGO NA VYAKULA VYA SAMAKI KUTOLEWA KWA NJIA YA KIELEKTRONIKI

DKT. MHEDE AONGOZA ZOEZI LA UCHANJAJI WA MIFUGO MKOANI IRINGA, WAFUGAJI WAPONGEZA HATUA YA SERIKALI

SERIKALI KURASIMISHA BIASHARA YA MABONDO