Nav bar

Ijumaa, 4 Aprili 2025

WATUMISHI WA LITA WAHIMIZWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA

Na. Stanley Brayton

◼️Ataka watumishi kufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina amewataka watumishi wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) kuzingatia Kanuni za Maadili ya Utumishi wa umma kwani taasisi yeyote ambayo haizingatii maadili ya Utumishi wa Umma ni vigumu sana kupata utendaji wenye tija.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe leo Aprili 04, 2025 Dodoma katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Mhina amesema kuna baadhi ya Watumishi wanashindwa kuzingatia Kanuni za maadili na Sheria za utumishi wa umma kutokana na uzembe na matokeo yake kuleta matokeo mabovu katika Taasisi.

"Tufanye kazi kwa bidii na kwa uaminifu kazini kwa kufuata misingi Mikuu ya Uadilifu, ikiwemo uwajibikaji na uaminifu," amesema Dkt. Mhina

Aidha, Dkt. Mhina amesema mtumishi anapaswa kutunza siri za ofisi kwa kutotumia taarifa za Serikali visivyo sahihi au bila idhini ya Utawala kwani Kanuni zinawataka kutunza taarifa kwa siri.

Vilevile, Dkt. Mhina ameitaka Menejimenti ya LITA kuwajengea watumishi wao uwezo na kuhakikisha wana utendaji mzuri kazi, na wanakuwa na uadilifu kwa kuzingatia Sheria na kanuni na Taratibu za Utumishi wa umma.

Dkt. Mhina amewapongeza LITA kwa mpangilio mzuri wa kampasi ambao zimekuwa zinatoa fursa mbalimbali zinazoonekana kwa wafugaji. 

Halikadhalika, Dkt. Mhina amesema bado kuna jukumu kubwa la kutoa mafunzo ya mifugo kwa wafugaji kwani chuo hakiwezi kuendelea kama hakiwekezi kwenye Miundombinu na ushirikishwaji wa jamii kwenye kutoa Mafunzo ya Mifugo.

Pia, Dkt. Mhina, ameipongeza Kamati ya Wajumbe wa Baraza Kuu LITA kwa kuendelea kujenga Vyuo vingine katika sehemu mbalimbali na amewataka Baraza kuisaidia Menejimenti katika kubuni Miradi mingine, ikiwa pamoja na kupima kama Mipango inaleta tija ambayo itaenda kufanya mabadiriko makubwa katika Taasisi baada ya miaka kadhaa ili kufanya maboresho makubwa zaidi.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene amesema wamepata nasaha kubwa kutoka kwa Mgeni Rasmi, na kuahidi kushirikishana katika Mipango yote ambayo imepangwa kwa Mwaka ujao wa fedha.

Dkt. Mwambene amesema wataendelea kuzingatia Maadili ya Utumishi wa Umma kwa kutekeleza Majukumu waliopewa na Serikali na kuwajibika ili kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na nchi nzima.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina, akitoa Hotuba katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene, akielezea Historia ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) pamoja na Mafanikio na Changamoto za Taasisi hiyo, katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) ambaye ni Naibu Mkuu wa Chuo Taaluma Utafiti na Ushauri LITA, Dkt. Anna Ngumbi, akitoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi (hayupo pichani), katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina (katikati) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene (kushoto), wakiimba wimbo wa  Mshikamano Daima wa Wafanyakazi wa LITA, katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma, kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi na Mkurugenzi  Msaidizi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Josephine Temihango (wa kwanza kulia), wakipitia Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Picha ni baadhi ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), wakiwa  katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) la Baraza hilo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina (katikati waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi hao wa LITA, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.















Hakuna maoni:

Chapisha Maoni