Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2024

WATAALAMU KUFANYA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA KUENDELEZA SEKTA YA NGOZI

Picha
Na. Stanley Brayton Wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Taasisi mbalimbali za kiserikali wamekutana kwa ajili ya kufanya tathimini ya utekelezaji wa mkakati wa kuendeleza Sekta ya ngozi kwa lengo la kuangalia ni namna gani utekelezaji wa Mkakati wa Tasnia hiyo umefikia ili kuweza kuuendeleza zaidi, ikiwa ni pamoja na kubaini mapungufu yake na kuangalia mambo ya kuzingatia ili kuenda katika hatua ya kuhuisha Mkakati huo uweze kuendana na wakati uliopo. Akizungumza, leo Novemba 28, 2024, mkoani Dodoma  katika kikao kazi cha Kamati ya Wataalamu cha kufanya Tathimini ya Utekelezaji wa Mkakati wa kuendeleza Sekta ya Ngozi, Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe - Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Nyamizi Bundala, amesema Tasnia ya ngozi ni moja ya tasnia muhimu hapa nchini inayotoa mchango mkubwa katika upatikanaji wa ajira, fedha za kigeni kutokana na mauzo ya ngozi nje ya nchi, na kuinua pato la wananchi pamoja na kuchangia katika Pato la Taifa kwa uju...

MABORESHO YA KANUNI ZA UVUVI ZA MWAKA 2009 KUSAIDIA KATIKA UWEKEZAJI

Picha
Na. Stanley Brayton Mkurugenzi wa Uvuvi Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Mohamed Ally Sheikh amesema maboresho haya ya Kanuni za Uvuvi za mwaka 2009 yatasaidia sana katika shughuli za uwekezaji ikiwa ni pamoja na kuwavutia wawekezaji wa nje na ndani katika tasnia ya uvuvi. Akizungumza, leo Novemba 19, 2024, mkoani Morogoro katika kikao cha kupitia Kanuni hiyo ili kubaini mapungufu na changamoto zake, Prof. Sheikh,  amesema mabadiriko haya ya kisheria yatasaidia sana katika shughuli za uwekezaji katika Sekta ya uvuvi hasa kwa kuwavutia wawekezaji kutoka nje na wawekezaji waliopo ndani ili kuwekeza katika sekta hiyo. "kitu tunachofanya sahivi hakiepukiki kwani ni kitu cha lazima, na ni lazima kufanya maboreaho ya hizi kanuni za Uvuvi ili kuendana na hali ya sasa" amesema Prof. Sheikh Aidha, Prof. Sheikh amesema viongozi wa ngazi za juu ya Serikali wanafanya juhudi kubwa katika kukuza biashara na kuweka mazingira mazuri ya biashara katika Sekta ya Uvuvi na hii inapelekea katika ...

WIZARA KUFANYA MABORESHO YA KANUNI ZA UVUVI ZA MWAKA 2009

Picha
 Na. Stanley Brayton Wataalamu Wizara ya Mifugo na Uvuvi wamekutana kwa ajili ya kupitia na kufanyia Maboresho Kanuni za Uvuvi za mwaka 2009 kwa kufanya uchambuzi na kuandaa Rasimu ya mapendekezo ya Kanuni mpya kwa kukusanya maoni ya wadau wa uvuvi ikiwa ni njia mojawapo ya kubaini mapungufu na changamoto zilizopo katika utekelezaji wake. Akizungumza, leo Novemba 18, 2024, mkoani Morogoro katika kikao cha kupitia Kanuni hiyo ili kubaini mapungufu na changamoto zake, Mkurugenzi Msaidizi wa Uthibiti Ubora, Viwango na Masoko ya Uvuvi - Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Christian Nzowa,  amesema kutokana na changamoto zinazojitokeza katika usimamizi wa rasilimali za uvuvi nchini, Wizara imekuwa ikifanya marekebisho ya Kanuni za Uvuvi za mwaka 2009 mara kwa mara ili kuingiza masuala yanayohitaji mabadiliko na kukabiliana na changamoto za kipindi husika. "kutokana na kukua kwa teknolojia na mabadiliko yanayojitokeza katika njia za mbinu za Uvuvi nchini, Imeonekana kwamba Kanuni za Uvuv...

TANZANIA NA CHINA KUSHIRIKIANA KATIKA TAFITI ZA UVUVI NA UFUGAJI SAMAKI KIIKOLOJIA KUPITIA TAFIRI

Picha
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe leo tarehe 11 Novemba, 2024 akiwa nchini China katika Jiji la Nanjing, Jimbo la JiangSu ametembele Taasisi ya Jiografia na Limnolojia ya Nanjing (Nanjing Institute of Geography and Limnology, Chinese Academy of Sciences, NIGLAS) ambayo inajihusisha na utafiti kwenye sayansi akua. Akiwa NIGLAS, Prof. Shemdoe amefanya mazungumzo na Menejimenti ya Chuo hicho na kukubaliana kushirikiana na Tanzania katika kazi za Utafiti wa Mambo ya Uvuvi na ufugaji samaki kiikolojia kupitia TAFIRI. Pia, Shemdoe amezipongeza NIGLAS na TAFIRI kwa kuendeleza mashirikiano ambayo yanaendeleza mahusiano kati ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Watu wa China ambayo yaliasisiwa na Mwl. Nyerere na Rais Mao Zedong.  Vilevile, Katibu Mkuu alikutana na kupokea taarifa ya mafunzo ya maabara yaliyotolewa kwa kipindi cha mwezi mmoja kwa watumishi wa kada ya Mafundi Sanifu Maabara kutoka TAFIRI. Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. R...