WATAALAMU KUFANYA TATHMINI YA UTEKELEZAJI WA MKAKATI WA KUENDELEZA SEKTA YA NGOZI
Na. Stanley Brayton Wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi na Taasisi mbalimbali za kiserikali wamekutana kwa ajili ya kufanya tathimini ya utekelezaji wa mkakati wa kuendeleza Sekta ya ngozi kwa lengo la kuangalia ni namna gani utekelezaji wa Mkakati wa Tasnia hiyo umefikia ili kuweza kuuendeleza zaidi, ikiwa ni pamoja na kubaini mapungufu yake na kuangalia mambo ya kuzingatia ili kuenda katika hatua ya kuhuisha Mkakati huo uweze kuendana na wakati uliopo. Akizungumza, leo Novemba 28, 2024, mkoani Dodoma katika kikao kazi cha Kamati ya Wataalamu cha kufanya Tathimini ya Utekelezaji wa Mkakati wa kuendeleza Sekta ya Ngozi, Mkurugenzi Msaidizi wa Mazao ya Mifugo, Usalama wa Chakula na Lishe - Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Nyamizi Bundala, amesema Tasnia ya ngozi ni moja ya tasnia muhimu hapa nchini inayotoa mchango mkubwa katika upatikanaji wa ajira, fedha za kigeni kutokana na mauzo ya ngozi nje ya nchi, na kuinua pato la wananchi pamoja na kuchangia katika Pato la Taifa kwa uju...