Nav bar

Jumamosi, 30 Septemba 2023

WAZIRI ULEGA AFANYA MAZUNGUMZO NA WATAALAM KUTOKA BENKI YA MAENDELEO YA AFRICA (AfDB)

 


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (katika) akiongea na timu ya Wataalam kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) (hawapo pichani) alipokutana nao mapema leo Septemba 27, 2023 jijini Dodoma kwa lengo la kufanya tathmini ya awali ya mradi wa Jenga Kesho Iliyobora (BBT) ambao Benki hiyo wanataka kuunga mkono. Kulia ni Katibu Mkuu, Prof. Riziki Shemdoe na kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Daniel Mushi. Mradi unatarajiwa kuanza Utekelezaji mapema mwezi Februari, 2024.


Kiongozi wa Mradi kutoka Taasisi ya Mabadiliko ya Kilimo Afrika (AATI), Bw. Marin VanDamme (kulia) akimuonesha jambo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati wa kikao kilichofanyika ofisini kwa Waziri huyo jijini Dodoma mapema leo Septemba 27, 2023. 

Lengo la kufika ofisini kwa Mhe. Waziri lilikuwa ni kuwasilisha hatua ya awali ya maandalizi ya Mpango Mkuu wa Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ili kupata maoni ya Mhe. Waziri kwa hatua iliyofikiwa kabla ya kuendelea hatua inayofuata.


Sehemu ya timu ya Wataalam kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na baadhi ya Wataalam kutoka Wizarani (pichani) wakifuatilia majadiliano wakati wa kikao baina yao na Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega kilichofanyika leo Septemba 27, 2023 jijini Dodoma kwa lengo la kufanya tathmini ya awali ya mradi wa Jenga Kesho Iliyobora (BBT) ambao Benki hiyo wanataka kuunga mkono.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akieleza jambo wakati wa kikao baina yake na timu ya Wataalam kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) (hawapo pichani) alipokutana nao mapema leo Septemba 27, 2023 jijini Dodoma.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni