Nav bar

Jumamosi, 30 Septemba 2023

MIFUGO NA UVUVI YAIBUKA KIDEDEA KAMBA WANAUME

Timu ya Wanaume kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeanza vema mbio zake za kutwaa ubingwa wa kuvuta kamba mara baada ya kuibuka na ushindi wa mivuto yote miwili dhidi ya timu ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi kwenye  mchezo uliochezwa leo Septemba 29, 2023 kwenye viwanja vya Chuo kikuu cha Mkwawa mkoani Iringa.


Muda mfupi ujao Wizara itatupa karata yake kwa upande wa mpira wa miguu ambapo itamenyana na timu ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera) kwenye uwanja wa chuo kikuu cha Mkwawa.

Timu ya mchezo wa kamba upande wa wanaume kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikimenyana na timu ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Lindi leo Septemba 29, 2023 ambapo iliibuka na ushindi wa mivuto yote miwili, Kulia ni mhamasishaji wa timu hiyo Bi. Mary Kamtole akitekeleza wajibu wake.

Hiki ndio Kikosi cha mchezo wa Kamba kwa upande wa wanaume kilichoibuka na ushindi dhidi ya timu ya Ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Lindi mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Chuo kikuu cha Mkwawa mkoani Iringa leo Septemba 29,2023 ikiwa ni sehemu ya michuano ya SHIMIWI inayoendelea mkoani hapa.

Pichani ni Kikosi cha timu ya mpira wa Pete kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi kinachocheza na timu ya Tume ya Utumishi muda mfupi ujao kwenye uwanja wa Chuo kikuu cha Ruaha leo septemba 29,2023 ikiwa ni muendelezo wa michuano ya SHIMIWI inayofanyika mkoani Iringa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni