Nav bar

Jumamosi, 30 Septemba 2023

MAADHIMISHO YA SIKU YA KICHAA CHA MBWA DUNIANI KITAIFA YAFANYIKA WILAYANI MPWAPWA

 

Mkurugenzi msaidizi Idara ya Huduma za Afya ya Mifugo Dkt.Stanford Ndibalema Mwakilishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Madhimisho ya ya siku ya Kichaa cha Mbwa Duniani  kitaifa Wilayani Mpwapwa akitoa Salamu za Wizara ambapo ameseama maadhimisho ya udhibiti wa Kichaa cha Mbwa nchini hufanyika kila mwaka kwa kushiikiana na Wizara ya Afya na wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kutoa elimu kwa jamii na wadau wa Mbwa na paka umuhimu wa kuchanja Mbwa ,(28.09.2023).

Wadau wa Mbwa na paka walioleta mbwa wao kwa ajili ya kuchanjwa wakimsikiliza mgeni rasmi  hayupo pichani akisoma hatuba ya maadhimisho ya siku ya  kichaa cha Mbwa duniani Wilayani Mpwapwa .(28.09.2023)

Mkurugenzi toka Wizara ya Afya Dkt.Rogati Kishimba akitoa salam za Wizara ya Afya kuhusu siku ya kichaa cha Mbwa duniani katika Madhimisho ya siku hiyo yaliyofanyika Wilayani Mpwapwa  leo ambapo amesema gharama za kutibu kichaa cha mbwa ni kubwa kuliko udhibi wa Ugonjwa huo hivyo jamii ihamasishwe kudhibiti ugonjwa huo.(28.09.2023).

Mgeni rasmi wa maadhimisho ya siku ya kichaa cha Mbwa Arb ogust Waryoba akitoa kadi kwa mbwa ambaye tayari amechanjwa kwa mwenye mbwa baada ya mbwa wake  kuchanjwa leo kwenye maadhimisho ya siku ya kichaa cha mbwa kitaifa Halmashauri ya Mpwapwa (28.09.2023)

Dkt. Wa Mifugo toka Halmashauri ya Mpwapwa Dkt.Emmanuel John akitoa chanjo kwa mmoja ya wafugaji w a Mbwa walioleta Mbwa wao kuchanjwa leo kwenye maadhimisho ya siku ya kichaa Mbwa kitaifa Wilayani Mpwapwa,(28.09.2023).

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni