Nav bar

Jumamosi, 30 Septemba 2023

KONGAMANO LA WADAU WA MAZIWA LAFANYIKA MKOANI MWANZA

 


Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania Dkt. George Msalya akitoa neno la utangulizi kwenye Kongamano la Wadau wa Maziwa mkoa wa Mwanza lilifanyika Septemba 26, 2023 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza ambapo ameelezea ukuaji wa Sekta ya Maziwa kwa ujumla hivyo amewataka wananchi wa Mwanza kuchangamkia fursa zilizopo kwenye Ufugaji hasa wa Ng'ombe wa Maziwa.


Mwakilishi wa Shirika la Heifer International Bw. Ndisha Joseph akijibu moja ya hoja iliyoibuka kwenye Kongamano la Wadau wa Maziwa lililofanyika Septemba 26, 2023 jijini Mwanza ambapo mmoja wa wajumbe alitaka kujua namna shirika hilo linavyoweza kuwasaidia wafugaji wadogo wadogo wa ng'ombe wa maziwa kupata elimu ili kufahamu faida ya kuwa katika vikundi vya Ushirika

Sehemu ya Washiriki wa Kongamano la Wadau wa Maziwa lililofanyika Septemba 26, 2023 Mkoani Mwanza wakifuatilia kwa makini mada mbalimbali zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye Kongamano hilo ambapo sehemu kubwa ya walioalikwa ni Wakuu wa Shule na Walimu Wakuu wa shule za Jiji la Mwanza, pamoja na mambo Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania Dkt. George Msalya amewapitisha kwa ufupi Mpango wa Unywaji Maziwa Shuleni uliozinduliwa hivi karibuni na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati wa Maadhimisho ya Wiki Ya Maziwa Juni 1, 2023 mkoani Tabora

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni