Nav bar

Jumamosi, 30 Septemba 2023

BOTI 4 ZENYE THAMANI YA 200M ZAKABIDHIWA KWA BMU's NKASI

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe leo tarehe 25 Sept 2023 amezindua na kukabidhi boti nne za doria zenye thamani ya 200M zilizotolewa msaada na taasisi ya The Nature Conservancy (TNC) kwa BMU's tisa zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mkoani Rukwa.


Akikabidhi boti hizo Prof.Shemdoe amesema kuwa boti hizo zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa, boti hizo ni kwaajili ya matumizi ya doria tu zisionekane tena  zinafanya kazi kinyume na malengo yaliyokusudiwa.


"Boti hizi nazizindua leo na kuwakabidhi, naomba sana zikatumike kwa ajili ya doria,zisionekane tena zinavua samaki huko ziwani, BMU's mnatakiwa kuwa waaminifu,mzitumie hizi boti kwa maslahi ya Jamii nzima inayowazunguka hapa". Alisema Prof.Shemdoe.


Aidha, Vijiji nufaika na Boti hizo ni pamoja na Kalungu, Mkinga, Kilando na Itete. Pia, Katibu Mkuu amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wa Wavuvi kote nchini, kwani katika Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa Rais ametoa jumla ya Boti 15 kwa ajili ya kukopesha vikundi vya Wavuvi kwa mkopo wa usiokuwa na riba.


Katika hatua nyingine, Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Taasisi ya The Nature Conservancy Bw. Peter Limbu amemweleza Katibu Mkuu kuwa mradi wa Uhifadhi wa Ziwa Tanganyika ni moja ya miradi Mingi inayotekelezwa nchini Tanzania kupitia shirika la kimataifa la Uhifadhi wa Mazingira (TNC).


Aidha, Limbu amesema kuwa katika Wilaya ya Nkasi Taasisi ya TNC inashirikiana na Shirika la "Sustain Lake Tanganyika" pamoja na jamii chini ya uongozi thabiti wa Wilaya ya Nkasi katika kulinda, Kutunza na kuendeleza rasilimali za ziwa Tanganyika ili ziweze kunufaisha jamii kwa chakula, biashara na maendeleo katika kizazi hiki na kijacho.


Awali Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mhe. Peter Lijualikali amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuwajali wananchi wa Wilaya ya Nkasi kwa kutoa Boti 15 kwa ajili ya kuwakopesha  Vikundi vya Wavuvi Wilayani Nkasi kwa mkopo usiokuwa na riba.


Vilevile Mhe.Lijualikali ameishukuru Taasisi ya The Nature Conservancy kwa kuwa mstali wa mbele wa kulinda na kuziendeleza rasilimali za Uvuvi katika ziwa Tan ganyika.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe  Pamoja na Mhe.Lijualikali, Mkuu wa Wilaya ya Nkasi,  wakikata utepe kuashiria kuzinduliwa kwa Boti 4 za doria ili ziweze kukabidhiwa kwa BMUs Katika Halmashauri ya Wilaya Nkasi.Wengine katika picha ni maafisa kutoka mkoa wa.Rukwa,  Halimshauri ya Wilaya ya Nkasi pamoja na wananchi.

Boti zilizokabidhiwa kwa  BMU's Katika Kijiji cha Kalungu Wilayani Nkasi kwa ajili ya Doria.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe (wa tatu kutoka kushoto) akimsikiliza Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Bw. Gerald Kusaya (Katikati) akiongea mara baada ya kufika ofisini kwake kusaini Kitabu cha Wageni.Wengine katika Picha ni timu ya Wataalam kutoka Mkoa wa Rukwa.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe akisalimia na baadhi ya wanakijiji cha Kalungu mara baada ya kuwasili kijijini hapo kwa ajili kukabidhi boti za doria kwa BMUs.Kulia kwake ni Mhe.Peter Lijualikali,Mkuu wa Wilaya ya Nkasi.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni