Nav bar

Ijumaa, 21 Julai 2023

ULEGA AZUNGUMZA NA WANANCHI WA KIJIJI CHA RUTORO WILAYANI MULEBA MKOANI KAGERA KWA AJILI YA KUTATUA MGOGORO

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akiongea na Wananchi wa Kijiji cha Rutoro (hawapo pichani) wakati wa ziara ya Mawaziri Nane wa Kisekta iliyolenga kutatua mgogoro katika Kijiji hicho cha Rutoro Wilayani Muleba, Mkoani Kagera Julai 20, 2023.

Timu hiyo ya Mawaziri nane iliongozwa na Mwenyekiti, ambaye ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Dkt. Angeline Mabula.
Mawaziri wengine walioshiriki katika ziara hiyo ni Naibu wa Waziri wa Kilimo, Mhe. Antony Mavunde, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja na Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Mhe. Khamis Hamza Chillo.







Hakuna maoni:

Chapisha Maoni