Nav bar

Ijumaa, 21 Julai 2023

KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AFUNGUA KIKAO CHA KWANZA CHA "OCEAN INNOVATION HUB" JIJINI DAR ES SALAAM.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe Jana tarehe 18 Julai, 2023 alifungua kikao cha kwanza cha kuanzisha TANZANIA OCEAN INNOVATIO HUB chini ya Marine Park Reserve Unit (MPRU) kwa kushirikiana  na Early Carrier Ocean Professionals (ECOP).


Aidha, lengo la kikao hicho ni kuwafanya vijana wawe sehemu ya wanufaikaji wa fursa za bahari na watatuzi wakuu wa changamoto za matumizi ya bahari. 


Pamoja na mambo mengine, Mhe. Maryvonne Pool, Balozi wa Seychelles nchini Tanzania alishiriki kikamilifu katika kikao hicho cha kwanza pamoja na washiriki wengine 30.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe, akisalimia na Balozi wa Seyshelles  Mhe.Maryvonne Pool, mara baada ya kumaliza kikao cha kwanza cha kuanzisha Tanzania Ocean Innovation Hub kilichofanyika jana tarehe 18July 2023 Jijini Dar es Salaam.

Picha mbalimbali za Washiriki wa kikao cha kwanza cha Tanzania Ocean Innovation Hub Kilichofanyika Jana tarehe 18 July 2023 jijini Dar es Salaam. Lengo la kikao hicho ni kuwafanya Vijana wawe sehemu ya Wanufaikaji wa fursa za Bahari na watatuzi wakuu wa Changamoto za Matumizi ya Bahari.

Picha ya Pamoja ya Katibu Mkuu   Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe (wa tatu kutoka kushoto) Wengine ni Dr.Immaculate Sware, Meneja wa MPRU, Balozi Maryvonne Pool, Dr. Leonard Valenzuela-Peres wa UN OCEAN Decade na Dkt. Kimirei, Mkurugenzi Mtendaji wa TAFIRI.

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe (Wa Pili kutoka kulia) akiwa na baadhi ya washiriki wa  Semina ya Ocean Innovation Hub Tanzania jana tarehe 18July, 2023 Jijini Dar es salaam.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni