Nav bar

Ijumaa, 30 Septemba 2022

ULEGA AMALIZA MKWAMO WA UTEKELEZAJI WA MRADI WA CHAMA CHA USHIRIKA CHA BUKASIGA

Na Martha Mbena.


Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) amemaliza mkwamo wa utekelezaji wa mradi wa ukaushaji dagaa wa chama cha Ushirika cha BUKASIGA uliopo katika kisiwa cha Ghana, Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe.


Mhe. Ulega alifanikiwa kuumaliza mkwamo huo wakati alipokuwa akiendesha kikao kazi cha kujadiliana namna bora ya kukubaliana kati ya chama cha Ushirika cha BUKASIGA, Sokoine University Graduates Entreprenuers Cooperative" (SUGECO) na Benki ya maendeleo ya Kilimo (TADB) kilichofanyika katika ukumbi wa mkutano, Jengo la Nbc,Dodoma. 22 Septemba 2022.


Mhe. Ulega amesema pande zote mbili wamefikia mahali pazuri na mwanga umeonekana na watu wamekubaliana kule ambapo wamepakusudia.


"Nawapongeza sana kwasababu washirika hawa wameitika wito wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwakuweza kufanya kazi kwa bidii kuweza kujenga uchumi wa nchi yetu" Amesema Mhe. Ulega.


Pia Mhe. Ulega ameagiza chama cha ushirika cha BUKASIGA  na watu wa SUGECO Kuandika mkataba wa makubaliano ambao utaeleza namna ya uendeshaji wa mradi na watu wa SUGECO, na kufikia makubaliano ambapo Wizara itasimamia makubaliano hayo, na ameagiza mwisho wa kuandaliwa mkataba huo  utakuwa tarehe 06 Oktoba 2022.


Naye  Mbunge wa Ukerewe, Mhe. Joseph Mkundi amemshukuru Mhe. Naibu Waziri kwa kuweza kuitisha kikao cha makubaliano na kuweza kuondoa mkwamo huo wa utekelezaji mradi wa ukaushaji dagaa, 


Mhe.Mkundi ameongezea kwa kusema anatamani kuona Bukasiga wanaendelea na mradi huo kwani waliweza kuhamasisha na vyama vidogovidogo kwenye zao la dagaa.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (Mb) akizungumza wakati wa kikao kazi cha kujadiliana na kupata namna bora ya kuondoa mkwamo wa utekelezaji wa mradi wa chama cha ushirika cha BUKASIGA, katika ukumbi wa mikutano Jengo la NBC, Dodoma, 22 Septemba 2022. (kushoto) ni Mbunge wa Ukerewe Bw. Michael Mkundi (kulia) ni Mkuu wa Wilaya ya Ukurewe Kanal Mhina.


Sehemu ya Washiriki waliohudhuria kikao kazi cha kuondoa Mkwamo wa utekelezaji wa mradi wa chama cha Ushirika cha Bukasiga, wakimsikiliza Naibu Waziri  wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye kikao hicho kilichofanyika Jengo la Nbc, Dodoma 22 Septemba 2022.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi , Mhe. Abdallah Ulega (Mb)  akiwa kwenye picha ya pamoja na washiriki ambao ni chama cha ushirika cha Bukasiga na watu wa (SUGECO) mara baada ya kumaliza kikao cha  kuondoa mkwamo wa utekelezaji wa mradi wa chama cha BUKASIGA. Dodoma, 22 Septemba 2022.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni