Nav bar

Jumanne, 30 Agosti 2022

WADAU TASNIA YA KUKU WAKUTANA KUJADILI CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI

Na Mbaraka Kambona, Arusha


Wadau wa tasnia ya kuku wamekutana kujadili changamoto zinazokabili mnyororo wa thamani wa tasnia ya kuku na kuweka vipaumbele vya uwekezaji kwa lengo la kuifanya tasnia hiyo kuwa na mchango mkubwa zaidi katika pato la taifa.


Wadau hao kutoka serikalini na sekta binafsi walikutana jijini Arusha Agosti 29, 2022.


Akifungua mkutano huo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki alisema pamoja na jitihada zinazoendelea kufanywa kukuza tasnia ya kuku bado tasnia hiyo inaonekana ni ndogo, hivyo aliwataka wadau hao kujadili kwa kina ni namna gani wafanye ili tasnia hiyo iwe na mchango unaotarajiwa.


"Kwa hiyo taarifa ya mnyororo wa thamani wa tasnia ya kuku mtakayoijadili leo mtaweza kuwa na majibu ya changamoto zilizopo katika kuifanya tasnia hii inakwama hasa katika eneo la afya ya kuku, biashara na masoko na kutafutia ufumbuzi changamoto hizo", alisema


Aliongeza kwa kusema kuwa pamoja na tasnia hiyo kuendelea kutoa mchango wake katika lishe na kipato bado wadau wanajukumu kubwa la kuhakikisha wanaongeza uzalishaji wa kuku na mayai ili kukidhi soko lililopo ndani na nje ya nchi.


Aidha, alisema kuwa serikali ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan imeendelea na itaendelea kuweke mazingira wezeshi kwa ajili ya tasnia ya kuku kukua huku akiwataka wadau hao kuendelee kutumia fursa hiyo kuimarisha mnyororo wa thamani wa tasnia hiyo kwa maslahi mapana ya taifa.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) akimueleza jambo Mwakilishi wa Benki ya Maendeleo ya Afrika(afDB), Bw. Salum Ramadhani (wa tatu kutoka kushoto) muda mfupi baada ya kufungua mkutano wa kujadili changamoto zinazokabili mnyororo wa thamani wa tasnia ya kuku na kuweka vipaumbele vya uwekezaji uliofanyika jijini Arusha Agosti 29, 2022.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki akiongea na wadau wa tasnia ya kuku (hawapo pichani) wakati akifungua mkutano wa kujadili changamoto zinazokabili mnyororo wa thamani wa tasnia ya kuku na kuweka vipaumbele vya uwekezaji uliofanyika jijini Arusha Agosti 29, 2022.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (katikati waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na Wadau wa tasnia ya kuku muda mfupi mara baada ya kufungua mkutano wa kujadili changamoto zinazokabili mnyororo wa thamani wa tasnia ya kuku na kuweka vipaumbele vya uwekezaji uliofanyika jijini Arusha Agosti 29, 2022.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni