Nav bar

Jumanne, 30 Agosti 2022

SEKTA YA MIFUGO YAFANYA MAZUNGUMZO NA MAKAMPUNI MAKUBWA YA NCHINI UINGEREZA

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayesimamia Sekta ya Mifugo amesema kuwa wameanza kufanya mazungumzo na Makampuni makubwa yanayojishughulisha na shughuli za mifugo ya nchini Uingereza.

 

Katibu Mkuu Nzunda ameyasema hayo leo (29.08.2022) baada ya kumalizika kwa mkutano uliofanyika kwa njia ya mtandao uliowashirikisha Viongozi kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania, baadhi ya Wadau wa Sekta ya Mifugo waliopo nchini Uingereza pamoja na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Sekta ya Mifugo, mkutano ambao ulifanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wizara uliyopo kwenye Mji wa Serikali – Mtumba Jijini Dodoma.

 

Mkutano huo ulijadili namna wadau hao kutoka nchini Uingereza wanavyoweza kuja kushirikiana na wadau wa Sekta ya Mifugo hapa nchini hasa wafuga ili kuikuza zaidi sekta hiyo.

 

Lengo hasa la mkutano huo ni kuona ni namna gani makampuni hayo yanaweza kusaidia kuimarisha mfumo wa ufugaji nchini kwa kutumia teknolojia rahisi za malisho ya mifugo, mbegu za mifugo na uchakataji wa mazao ya mifugo.

 

Katika mkutano huo makampuni hayo yameonyesha baadhi ya teknolojia za uchakataji wa malisho, ngozi, nyama na maziwa. Serikali imeyakaribisha makampuni hayo kwa ajili ya kuja kuleta teknolojia rahisi na yenye bei nafuu ili kuwezesha wafugaji wadogo na wa kati kumudu gharama za vifaa na kuzalisha kwa tija.

 

Lakini pia kupitia teknolojia hizi, zitasaidia kujenga uwezo wa Wizara katika kutambua teknolojia mbalimbali zinazotumika na nchi zilizoendelea kama Uingereza kwa ajili ya kuendeleza Sekta ya Mifugo.

 

Naye Mshauri Biashara kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania, Godfrey Lwakatare amesema kuwa lengo la kufika Wizarani ni kuiunganisha Sekta ya Mifugo na Makampuni makubwa kutoka nchini Uingereza yanayojishughulisha na sekta ya mifugo. Matarajio yao ni kuwa Sekta ya Mifugo hapa nchini itaweza kukua kupitia ushirikiano huo na Sekta Binafsi.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda akifungua mkutano uliofanyika kwa njia ya mtandao uliowashirikisha Viongozi kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania, baadhi ya Wadau wa Sekta ya Mifugo waliopo nchini Uingereza pamoja na Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Sekta ya Mifugo ambao ulijadili namna wadau hao kutoka nchini Uingereza wanaweza kuja kushirikiana na wadau wa Sekta ya Mifugo hapa nchini hasa wafuga ili kuikuza zaidi sekta. Kushoto ni Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu (Mifugo), Dkt. Charles Mhina na kulia ni Mshauri Biashara kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania, Godfrey Lwakatare. Mkutano huo umefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wizara iliyopo kwenye Mji wa Serikali – Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)


Baadhi ya Viongozi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Mifugo) na Viongozi kutoka Ubalozi wa Uingereza nchini Tanzania wakifuatilia mada zilizokuwa zikiwasilishwa kwenye mkutano uliowashirikisha wadau wa Sekta ya Mifugo nchini Uingereza, ulijadili namna wadau hao kutoka nchini Uingereza wanaweza kuja kushirikiana na wadau wa Sekta ya Mifugo hapa nchini hasa wafuga ili kuikuza zaidi Sekta hiyo. Mkutano huo umefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wizara uliyopo kwenye Mji wa Serikali – Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Sera na Mipango, Bw. Mbaraka Stambuli akiwasilisha mada ya fursa zilizopo kwenye Sekta ya Mifugo wakati wa mkutano uliofanyika kwa njia ya mtandao ulijadili namna wadau wa Sekta ya Mifugo kutoka nchini Uingereza wanaweza kuja kushirikiana na wadau wa Sekta ya Mifugo hapa nchini hasa wafuga ili kuikuza zaidi sekta hiyo. Mkutano huo umefanyika kwenye ukumbi wa Ofisi ya Wizara uliyopo kwenye Mji wa Serikali – Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda (kushoto) akimuelezea Waziri wa Nchi, Umwagiliaji na Nyanda za Chini, Mhe. Dkt. Birhanu Megersa kutoka nchini Ethiopia (hayupo pichani) namna Sekta ya Mifugo ilivyojipanga kuhakikisha mchango wa sekta hiyo kwa wafugaji na pato la Taifa unakua. Mazungumzo hayo yalifanyika kwenye Ofisi za Wizara zilizopo kwenye Mji wa Serikali - Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)


Waziri wa Nchi, Umwagiliaji na Nyanda za Chini, Mhe. Dkt. Birhanu Megersa kutoka nchini Ethiopia akielezea mambo mbalimbali aliyojifunza kwenye ziara yake ya kujifunza namna Tanzania ilivyojipanga kwenye matumizi na uendelezaji wa maeneo ya wafugaji wa asili. Mazungumzo hayo yalifanyika kwenye Ofisi za Wizara zilizopo kwenye Mji wa Serikali - Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda akizungumza na Viongozi na Wataalam kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Mifugo wakiongozwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hiyo, Dkt. Jimmy Smith (wa pili kulia) walipofika ofisini kwake kwa lengo la kuona ni namna gani Taasisi wanazofanya nazo kazi zinafanikiwa, changamoto na kama kuna maeneo ambayo baadae yatahitaji kufanyiwa tafiti. Mazungumzo hayo yalifanyika kwenye Ofisi za Wizara zilizopo kwenye Mji wa Serikali - Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)


Picha ya pamoja ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Bw. Tixon Nzunda (wa nne kutoka kulia) akipokea zawadi kutoka kwa Viongozi na Wataalam wa Taasisi ya Kimataifa ya Utafiti wa Mifugo mara baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika kwenye Ofisi za Wizara zilizopo kwenye Mji wa Serikali - Mtumba Jijini Dodoma. (29.08.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni