Nav bar

Ijumaa, 26 Agosti 2022

MKUTANO NA WAWEKEZAJI WA KAMPUNI YA BLUE CHELE CHELE KUTOKA NCHI YA SHELISHELI

 


Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi Bw. Magese Bulayi (katikati) akiongoza mkutano na wawekezaji wa Kampuni ya BLUE CHELE CHELE kutoka nchi ya Shelisheli hawapo pichani. Lengo la mkutano huo ni kujadili na kukubaliana maeneo ambayo wanaweza kuwekeza katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari  na Mwambao wa Bahari ya Hindi katika  Sekta ya Uvuvi. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Viumbe Maji Bw. Nazaeli Madala na Kushoto ni Muwakilishi kutoka Mamlaka ya Uvuvu wa Bahari Kuu (DSFA) BW. Peter Shunula. Mkutano huo umefanyika MVUVI HOUSE - Dsm,  (18.08.2022)


Balozi wa Heshima kutoka Jamhuri ya Shelisheli Bi. Màryvonne Pool (kushoto) akiongoza msafara huo wa wawekezaji kutoka SheliSheli amefuatana na Muwekezaji kutoka  Kampuni ya BLUE CHELE CHELE Bw. Danny Lowman (katikati)na Mshauri Muelekezi Bi. Sheryl Vangadasamy katika mkutano huo. (18.08.2022)


Kikao na Wawekezaji kutoka SheliSheli kimehudhuriwa na Wataalamu kutoka Idara ya Uvuvi (HQ), TAFIRI, MPRU, DSFA, TAFICO na Maafisa Wafawidhi wa Kanda Kuu ya Pwani na Mashariki. (18.08/2022)


Picha ya pamoja na Mkurugenzi wa Idara ya Uvuvi Bw. Magese Bulayi(wa tatu kulia) akifuatiwa na Balozi wa Heshima Bi. Martvonne Pool,  akifuatiwa na Mshauri Muelekezi Bi Sheryl Vangadasam kutoka Jamhuri ya Shelisheli, Kaimu Mkurugenzi wa TAFICO Bi. Ester Mndeme, Mkurugenzi  Idara ya Ukuzaji wa Viumbe Bw. Nazael Madala na Muwekezaji kutoka Kampuni ya BLUR CHELE CHELE Bw. Danny Lowman. Kulia ni Mkurugenzi TAFIRI Bw. Eshmael Kimirei na Bi. Anita Kutoka MPRU, mara baada ya kumaliza kikao na wawekezaji katika Sekta Ya Uvuvi hapa nchini (18.08.2022)

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni