Nav bar

Jumatatu, 15 Oktoba 2018

ULEGA AFUNGUA RASMI MAONESHO YA NNE YA NDEGE WAFUGWAO




Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi na Mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega amezindua rasmi maonesho ya nne ya ndege wafugwao katika viwanja vya maonesho (sabasaba) jijini Dar es salaam.


Akizungumza katika uzinduzi huo Ulega ameeleza kuwa maonesho ya mwaka huu yamehusisha makampuni mengi ya ndani na nje ya nchi kama Kenya, Poland na China na amewakaribisha kuwekeza nchini kutokana na kuwepo kwa fursa za uwekezaji katika sekta mbalimbali.


Aidha ametoa pongezi kwa vyama vyote vya wadau wa ndege wafugwao chini ya chama mama cha Tanzania Poultry show (TPS) kwa kutoa kipaumbele katika suala la ufugaji wa kuku.


Pia amewataka kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja na wao kama serikali wapo pamoja kama walezi wao, katika kuhakikisha wanasonga mbele zaidi na amewapongeza kwa ushirikiano wao kupitia vyama vyao.


Ulega amesema kuwa Rais Magufuli ameendelea kusimamia maendeleo ambapo hadi sasa tozo zilizokuwa kero kwa wafugaji, wakulima na wavuvi zimeondolewa ili kuweza kuendeleza shughuli hizo.


 Kuhusiana na changamoto zilizotolewa na wafugaji hao hasa katika mashudu na soya ambazo huagizwa kutoka nje Ulega amesema kuwa maandalizi yameanza katika nyanda za juu kusini ambako soya zimelimwa na wanavutia uwekezaji katika usindikaji ili kuweza kuvutia uwekezaji wa kuchakata soya na kupunguza gharama za kuagiza bidhaa hizo kutoka nje.


Kuhusiana na machinjio zinazochinja kuku Ulega amesema kuwa sehemu hizo zimekuwa na ubora wa chini sana na amewataka wahakikishe wanaboresha machinjio hayo yanayosimamiwa na halmashauri na manispaa hasa kwa kuzingatia wanaweka  sehemu ya machinjio ya kuku ili kuleta thamani.


Mwenyekiti wa chama cha ndege wafugwao Harko Bhaghat amemshukuru Naibu Waziri na Wizara kwa ujumla kwa kutoa kipaumbele kwa wafugaji na kusema kuwa hadi sasa wamepata mafanikio makubwa na kubwa zaidi ni baada ya serikali kuondoa tozo katika bidhaa za mifugo.


Bhaghati amewataka wafugaji kujisajili ili waweze kupata fursa mbalimbali za kuendeleza soko la ndege wafugwao hasa kuku.


Mtaalamu na Mshauri wa Mifugo kutoka kampuni ya Hill Poultry Feed akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega kuhusu uzalishaji na utunzaji wa mifugo unaofanywa

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi ,Abdallah Ulega akizungumza na wafugaji wa ndege wafugwao katika ufunguzi wa maonesho ya nne ya ndege wafugwao nchini jijini  Dar es salaam.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akitembelea mabanda mbalimbali katika viwanja vya sabasaba jijini Dar es salaam




Hakuna maoni:

Chapisha Maoni