Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2018

NAIBU WAZIRI MHE. ABDALLAH ULEGA AIAMBIA KAMATI YA BUNGE KUWA SERIKALI INA MTAZAMO WA KUIFANYA SEKTA YA MIFUGO NA UVUVI KUWA SEKTA YA UZALISHAJI - KIGOMA

Picha
Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdalah Hamis Ulega ambaye  ni Mbunge wa Jimbo la Mkuranga ameiambia kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji kuwa, Serikali ina mpango wa kuifanya sekta ya Mifugo na Uvuvi kuwa na mchango mkubwa katika pato la Taifa.   Naibu Waziri Hamisi Ulega ameyasema hayo leo Mkoani Kigoma mbele ya Kamati ya kudumu ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji, ilipokuwa katika ziara ya kutembelea   chuo cha wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA)   kampasi ya kigoma jana. Mhe. Ulega amesema   Wizara yake ina Mkakati   wa kulinda rasilimali za Mifugo na Uvuvi, kwa kuimarisha uvuvi wa bahari kuu na kuitoa sekta hiyo   kwenye kuchangia kiasi na shilingi Bilioni 19 kwa   mwaka katika pato la taifa hadi kufikia kuchangia zaidi ya shilingi Bilioni 50 kwa mwaka. “Tunaweza kufikia malengo haya kwanza kwa kuimarisha uvuvi wa Bahari kuu kwa kuhakikisha kwanza tasisi yetu ya kusimamia uvuvi wa bahari kuu inakuwa...

MNADA WA UPILI WA PUGU KUWA MNADA WA KIMATAIFA-LUHAGA MPINA

Picha
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe Luhaga Joelson Mpina amesema kuwa mnada wa pugu utakarabatiwa na  kuwa mnada wa kimataifa utakaokuwa unahudumia wafanyabiashara kutoka nchi yoyote Africa na duniani kwa ujumla. Tanzania Mungu ametujalia kuwa na tunu ya Rasilimali ng'ombe,Nchi zilizoendelea wanajivunia  vitu vyao,Mfano viwanda,ifike wakati na Sisi tujivunie Rasilimali ng'ombe tuyoliyopewa Mungu Bure. "Haiwezekani Sisi Tanzania tuwe wa pili africa kuwa na Mifugo mingi,tukitanguliwa na nchi ya Ethiopia halafu tukose kuwa  na mnada wa kimataifa" Mpina ameyasema hayo Leo alipofanya ziara ya kukagua eneo la mnada huo lililovamiwa na wananchi na kujionea hali halisi ya uvamizi wa  eneneo hilo. Pia baada ya kuzungu na kukagua eneo la mnada huo na kushuhudia uvamizi mkubwa uliofanyika katika eneo hilo,Mhe.Mipina ameunda timu maalumu itakayopita nyumba baada ya nyumba kuchunguza na kuhoji uhalali wao wa kuwepo katika eneo la Serikali na kujiridhi...

WAZIRI MPINA APOKEA MADUME 11 YA NG'OMBE BORA KATIKA KITUO CHA NAIC - ARUSHA

Picha
Mhe.Waziri Luhaga Mpina akiwa na Katibu Mkuu Mifugo Dkt. Maria Mashingo akikata utepe kuashiria kupokelewa kwa Madume hayo ya Mbegu Maelekezo ya Mhe. Waziri wakati alipokuwa akipokea madume ya ng'ombe bora 11 ya mbegu katika Kituo cha Uzalishaji Mifugo kwa Chupa (NAIC) Arusha. 1.Amemshukuru na kumpongeza KMM kwa kazi kubwa ya kuhakikisha utoshelevu wa mbegu za AI kwa kuwepo kwa jumla ya madume bora 26 hadi sasa yenye uwezo wa kuzalisha jumla ya dozi 3,120,000 kwa mwaka. 2.Amemuagiza KMM kuandaa mpango maalum wa kuhimilisha Ng'ombe Milioni moja wa maziwa.Mpango huo uanze kutekelezwa katika bajeti ya mwaka huu(2018/19).  3.Pia Mhe. Waziri amemuagiza KMM kufanya tathmini ya kuona kama kuna haja  au umuhimu wa kuagiza maziwa na mazao yake nje ya nchi.Tathimini hiyo inatakiwa kukamilika katika kipindi cha wiki mbili kuanzia sasa.  4.Aidha Mhe. Waziri amemuagiza KMM  kufanya tathmini ya kuona kama maziwa na mazao yake yanayoingizwa...

WANAOAGIZA NYAMA, MAZIWA NA SAMAKI KUTOKA NJE YA NCHI SIKU ZAO ZAHESABIKA - ULEGA KIGOMA

Picha
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalah Ulega, amesema kuwa wanaoagiza nyama, maziwa na samaki kutoka nje ya nchi, siku zao zahesabika kutokana na nchi kuwa na mifugo ya kutosha kama vile Ngombe, Mbuzi, Kondoo, Kuku na Punda. Hivyo, Taifa kama Tanzania halina sababu yoyote ya kuagiza mazao hayo ya mifugo na uvuvi kutoka nje ya nchi. Naibu waziri Ulega aliyasema hayo alipokuwa katika ziara ya siku tatu Mkoani Kigoma ya kutembelea Mwalo wa Samaki wa Muyobozi Uliyopo Wilayani Uvinza na Mwalo wa Kibirizi na kituo cha Taasisi ya Tafiti za Uvuvi Tanzania TAFIRI Kigoma. “Sioni kwanini tuagize nyama na maziwa   toka nje   ya nchi, hatuwezi kuendelea kuangiza nyama, maziwa na hata mazao ya uvuvi, kwa nini tusiwekeze katika rasilimali zetu za ndani   katika mifugo na samaki na kuongeza pato la taifa? “Aliuliza Ulega. Ulega   aliongeza kwa kusema kuwa Wizara yake haitawavumilia   wafanyabiashara wanaoagiza nyama, maziwa na mazao ya samaki   toka nje y...