Nav bar

Jumanne, 19 Desemba 2017


NAIBU WAZIRI ULEGA AKAMATA TANI 11 ZA SAMAKI WALIOKUWA WAKITOROSHWA BILA KULIPIWA USHURU WA TSH. 99,000,000/=

Na Kumbuka Ndatta

Naibu Waziri wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdalla Ulega amekamata tani 11 za Samaki aina ya Sangara katika soko la kimataifa la Mwaloni jijini Mwanza waliokuwa wakitoroshwa bila kuliopiwa wa ushuru wa Tsh.99,000,000 kwenda nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo hivi karibuni

Samaki hao walikuwa wakitoroshwa na wafanyabishara kutoka nchini Kongo waliokuwa na kibali kinachoonyesha  wanaenda kuuzwa Tunduru Mkoani Ruvuma.

 “Jamani naomba msimamie sheria ili kulinda rasilimali zetu zisitoroshwe kwenda nje bila kulipiwa kodi. Lazima tumuunge mkono Rais wetu John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Rasilimali hizi ziwanufaishe wananchi na sio watu wachache”alisisitiza wakati akiongea na uongozi wa Manispaa ya Ilemela.

Ulega amesema kuwa ni kinyume cha sheria kuvua samaki wachanga na wazazi, na ameuagiza uongozi wa Manispaa ya Ilemela kupitia Mkurugenzi wake Bw.John Wanga kusimamia sheria ipasavyo ili kudhibiti kuvuliwa kwa samaki wasioruhusiwa kisheria.

“Ikitokea wakati wa ukaguzi wenu mmekamata Samaki wachanga au wazazi taifisheni na sheria ichukue mkondo wake mara moja kwa yeyote anayehusika au anayevunja sheria kwa kujua au kutokujua”alisema Ulega.

Akihutubia wafanyabiashara katika soko la Mwaloni jijini Mwanza, Waziri Ulega alielezwa changamoto wanazokumbana nazo ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji safi na salama na ubovu wa miundombinu ya vyoo katika soko hilo.

Mhe.Ulega amempa siku tatu Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemele Bw.John Wanga kuhakikisha maji na Miundombinu ya vyoo sokoni hapo inashughulikiwa ndani ya siku tatu, hadi ifikapo Disemba 18, 2017.


Mhe. Naibu Waziri Abdallah Ulega ashika Tani 11 ya samaki waliokuwa wakitoroshwa bila kulipwa ushuru

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni