Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2017

KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI (MIFUGO) DKT MASHINGO AFANYA ZIARA MKOANI TABORA KATIKA MNADA WA UPILI IPULI TAREHE 23/09/2017

Picha
 Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi  (Mifugo)  Dkt. Maria Mashingo afanya ziara katika mnada wa upili Ipuli Manispaa ya Tabaora (Secondary Market).Lengo kubwa la ziara hiyo ilikuwa kujiridhisha na changamoto zilizopo katika mnada huo ambapo Manispaa ya Tabora wanaomba uhamishiwe eneo lingine. Aidha Manispaa ya Tabora imeomba mnada wa Ipuli uhamishiwe eneo lingine  kwa sababu eneo ulipo sasa umezungukwa na makazi ya watu.Vile vile  Manispaa ya Tabora  imependekeza mnada huo urudishwe kuwa mnada wa awali ili uendeshwe na Manispaa ya Tabora. Septemba 22 mwaka huu Katibu Mkuu Mifugo alifanya kikao na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe .Agrey Mwanry kujadili namna bora ya kuweza kuuhamisha mnada huo na kuupeleka nje kidogo ya mji wa Tabora,lengo ikiwa ni kuuboresha mnada huo ambao kwa sasa umezungukwa na Makazi ya watu. Awali katibu Mkuu Mifugo alikutana na kujadiliana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Maeneo  bora ya kuhamishia mnada huo.Katibu...

MASHINDANO YA KUVUA SAMAKI YALIYOFANYIKA TAREHE 10/09/2017 JIJINI DAR ES SALAAM

Picha
Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi Bi. Fatma Sobo kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Uvuvi akitoa neno kwa wavuvi katika mashindano hayo yaliyofanyika BMU Msasani Bw. Ally mshindi wa 3 katika mashindano ya uvuvi alipatiwa zawadi na Bi. Fatma Sobo (Kaimu Mkurugenzi) yenye thamani ya Tshs laki tano picha ya pamoja na wavuvi Pichani ni mshindi wa kwanza Bw. Issa alievua samaki kilo 75 ambapo alipewa zawadi yenye thaman ya tshs milioni nne na lakitatu kutoka kampuni ya YAMAHA pamoja na zawadi nyingine kutoka Wzarani Bw. Mohamed Omari mshindi wa pili alipatiwa zawadi yenye thamani ya tshs milioni moja na elfu hamsini

KATIBU MKUU MIFUGO ATEMBELEA ENEO LA UFUGAJI MWISA II MULEBA MKOANI KAGERA

Picha
Kaimu Mkurugenzi Idara ya uzalishaji na masoko Bw.Victor Mwita akifafanua jambo kwenye mkutano uliofanyika ofisini kwa Mkuu wa wilaya (DC) ya Muleba Mkoani Kagera Katibu Mkuu Idara kuu ya Mifugo Dkt. Mary Mashingo akitoa ufafanuzi wa baadhi ya hoja zilizoibuliwa na DC pamoja na mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Muleba Katibu Mkuu Dkt. Mary Mashingo akiwa na timu ya wataalam akionyeshwa baadhi ya ``BICON" ya mpaka eneo la Mwisa II Katibu Mkuu na baadhi ya wataalamu wakiangalia moja ya Rambo linalochimbwa kwa nguvu ya wananchi katika kijiji cha Itunzi Katibu Mkuu Dkt. Mary Mashingo akipokea maelezo kutoka kwa mtaalam wa ardhi Bw. Kafero kutoka Mkoani Kagera

HOTUBA YA NANENANE ILIYOWASILISHWA NA MHE. WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI DKT. CHARLES TIZEBA ILIYOFANYIKA LINDI 2017

Picha
Mhe. Dkt. Charles Tizeba HOTUBA YA WAZIRI WA KILIMO MIFUGO NA UVUVI MHE, MHANDISI, DKT. CHARLES JOHN TIZEBA (MB) WAKATI WA KUMKARIBISHA MGENI RASMI KATIKA KILELE CHA MAADHIMISHO YA SIKUKUU YA WAKULIMA, NANE NANE KITAIFA, VIWANJA VYA NGONGO KATIKA MANISPAA YA LINDI TAREHE 8/8/2017 Mheshimiwa, Mgeni Rasmi, Makamu wa   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan Waheshimiwa Mawaziri wa Tanzania Bara na Visiwani, Makatibu Wakuu wa Tanzania Bara na Visiwani, Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa ya Tanzania Bara, Makatibu Tawala wa Mikoa, Mhe. Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo Mifugo na Maji Waheshimiwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Mameya na Wenyeviti wa Halmashauri mliopo, Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya, Miji na Majiji, Wataalamu wa Kilimo, Mifugo, Uvuvi na Ushirika, Wanahabari wa Vyombo mbalimbali, Wageni Waalikwa, Mabibi na Mabwana, ...

WATAALAMU WA MIFUGO WATEMBELEA MKOA WA KAGERA KWA AJILI YA KAZI MAALUM YA KUAINISHA NA KUPIMA ENEO LA MWISA TAREHE4/09/2017

Picha
                             ENEO LA MWISA II KUAINISHWA NA KUPIMWA Wataalamu wa mifugo kutoka Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi (Idara kuu ya Mifugo) wamewasili Mkoani kagera kwa ajili ya kazi maalum ya kuainisha na kupima eneo la Mwisa II. Eneo la Mwisa II linakadiriwa kuwa na hekta zisizopungua 50,000 ni miongoni mwa maeneo yanayoangukia chini ya ukanda wa ufugaji ambao unaanzia mpakani mwa nchi ya Uganda hadi katika pori la akiba la Burigi katika ziwa Burigi  Wilaya ya Muleba na Karagwe Mkoani Kagera. Ili kuhakikisha kazi hii ya Uainishaji na upimaji wa eneo la Mwisa II inafanyika kwa ufanisi mkubwa wataalamu kutoka Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi (Idara kuu ya Mifugo) watashirikiana na Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi, OR - TAMISEMI (Mkoa na Wilaya) pamoja na NARCO. Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi kupitia Idara...