KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO MIFUGO NA UVUVI (MIFUGO) DKT MASHINGO AFANYA ZIARA MKOANI TABORA KATIKA MNADA WA UPILI IPULI TAREHE 23/09/2017
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Dkt. Maria Mashingo afanya ziara katika mnada wa upili Ipuli Manispaa ya Tabaora (Secondary Market).Lengo kubwa la ziara hiyo ilikuwa kujiridhisha na changamoto zilizopo katika mnada huo ambapo Manispaa ya Tabora wanaomba uhamishiwe eneo lingine. Aidha Manispaa ya Tabora imeomba mnada wa Ipuli uhamishiwe eneo lingine kwa sababu eneo ulipo sasa umezungukwa na makazi ya watu.Vile vile Manispaa ya Tabora imependekeza mnada huo urudishwe kuwa mnada wa awali ili uendeshwe na Manispaa ya Tabora. Septemba 22 mwaka huu Katibu Mkuu Mifugo alifanya kikao na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe .Agrey Mwanry kujadili namna bora ya kuweza kuuhamisha mnada huo na kuupeleka nje kidogo ya mji wa Tabora,lengo ikiwa ni kuuboresha mnada huo ambao kwa sasa umezungukwa na Makazi ya watu. Awali katibu Mkuu Mifugo alikutana na kujadiliana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Maeneo bora ya kuhamishia mnada huo.Katibu...