Nav bar

Jumatano, 6 Machi 2024

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI MHE. ABDALLAH ULEGA AONGEA NA WAFANYABIASHARA WA MAZAO YA SAMAKI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akiongea na wavuvi na wafanyabiashara wa mazao ya samaki wa soko la Kilumba alipowatembelea kuzungumza nao Januari 29, 2024 kuhusu ujio wa Mhe. Rais na hafla ya Ugawaji Boti na Vizimba kwa Wavuvi wa Ziwa Viktoria tukio litakalofanyika katika uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza Januari 30, 2024. Mgeni rasmi wa tukio hilo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan. Kulia ni Katibu Mkuu, Prof. Riziki Shemdoe. Kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Bi. Agnes Meena.

Sehemu ya Wavuvi na Wafanyabiashara wa mazao ya samaki wa soko la Kilumba wakimsikiliza Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (hayupo pichani) alipowatembelea kuzungumza nao Januari 29, 2024 kuhusu ujio wa Mhe. Rais na hafla ya Ugawaji Boti na Vizimba kwa Wavuvi wa Ziwa Viktoria tukio litakalofanyika katika uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza Januari 30, 2024. Mgeni rasmi wa tukio hilo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akiongea na Wakina mama ambao ni Wafanyabiashara wa samaki wa Kamanga Feri alipowatembelea kuzungumza nao leo Januari 29, 2024 kuhusu ujio wa Mhe. Rais na hafla ya Ugawaji Boti na Vizimba kwa Wavuvi wa Ziwa Viktoria tukio litakalofanyika katika uwanja wa Nyamagana, jijini Mwanza Januari 30, 2024. Mgeni rasmi wa tukio hilo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Pichani ni sehemu ya Vizimba vinavyotarajiwa kugawiwa kwa wavuvi wa Ziwa Victoria.

 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni