Nav bar

Jumatano, 6 Machi 2024

ULEGA AITAKA NHC KUTUMIA MALIGHAFI ZA NDANI

 

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega amelitaka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambaye ndio Mkandarasi wa ujenzi wa jengo la Ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi linalojengwa katika mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma kuhakikisha wanatumia malighafi zinazozalishwa na viwanda vilivyopo hapa nchini.

Ulega ametoa maelekezo hayo alipofanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo leo Januari 7, 2024 ambapo aliambatana na timu ya Wataalamu wa Wizara.

“Nimekagua hapa nimeona vipo vinavyozalishwa hapa nyumbani na nyinyi ni shirika la kizalendo lakini ajabu sana mmeacha kununua vitu vya hapa nyumbani mmeamua kwenda kununua vilevile ambavyo vinapatikana hapa nchini, na mkumbuke hamjengi nyumba ya mtu binafsi ni ya umma”, alisema

Mhe. Ulega ametoa rai kwa shirika hilo kama wanachofuata huko nje ni ubora au mtindo, wakutane na wazalishaji waliopo hapa nchini na kuwaelekeza ubora na mitindo wanayoitaka ili waweze kuzalishiwa.

Aidha, Waziri Ulega amemtaka Mshauri Elekezi wa jengo hilo (TBA) kuhakikisha anamaliza ujenzi huo Mei 31, 2024 kama mkataba unavyowataka.


Fundi Mkuu, kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Injinia, Remigius Mwijage akimpa maelezo ya mchoro wa jengo Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega alipofanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi unaondelea katika Mji wa Serikali Mtumba, jijini Dodoma leo Januari 7, 2024.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega (kushoto) akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Sera na Mipango, kutoka Wizara ya Ardhi na Mendeleo ya Makazi, Bw. Amos Zephania (wa pili kutoka kulia) na Mshauri Mwelekezi wa Ujenzi wa Jengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Injinia, Weja Ng’olo alipofanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo leo Januari 7,2024. Wa pili kutoka kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Daniel  Mushi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na Watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Mkandarasi pamoja na Mshauri Mwelekezi wa Ujenzi wa Jengo la Wizara ya Mifugo na Uvuvi alipofanya ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa jengo hilo leo Januari 7,2024. Wa pili kutoka kushoto ni Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni