Nav bar

Jumapili, 5 Julai 2020

MAKATIBU WAKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WATEMBELEA MAONESHO YA SABASABA


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kwenye Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo (5/7/2020)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akipokea Zawadi kutoka kwa Florence Mahimbo wa Kampuni ya Bigfish wakati alipotembelea Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo (5/7/2020)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akipata maelezo kutoka kwa Mtafiti wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI), Bi. Neema Urassa wakati alipotembelea Monesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo (5/7/2020)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatamah akitoa ushauri kuhusu ufugaji wa Samaki kwa kutumia matanki wakati alipotembelea banda la SUMA JKT kwenye Maonesho ya 44 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea kwenye Viwanja vya Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo (5/7/2020)



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akiwa na Afisa Masoko wa Kampuni ya AKM Glitters, Jackson Kaheza alipotembelea Kampuni hiyo inayofanya shughuli zake jijini Dar es Salaam mapema leo Julai 5, 2020.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Elisante Ole Gabriel akisaini Kitabu cha Wageni alipotembelea banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Kimataifa ya 44 ya biashara (Sabasaba) yanayofanyika kwenye Uwanja wa Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo Julai 5, 2020. Kushoto anayeshuhudia ni Mratibu wa Maonesho wa Wizara hiyo, Mary Yongolo.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel akimsikiliza Mtangazaji wa TBC1, Vumilia Mwasha wakati wa Mahojiano katika banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi lililopo katika Maonesho ya Kimataifa ya 44 ya biashara ya (Sabasaba) yanayofanyika kwenye Uwanja wa Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Da es Salaam leo Julai 5, 2020.



Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel (kushoto) akiangalia malisho ya mifugo katika banda la Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI) lilipo ndani ya banda la Wizara ya Mifugo na Uvuvi katika Maonesho ya Kimataifa ya 44 ya biashara (Sabasaba) yanayofanyika kwenye Uwanja wa Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam leo Julai 5, 2020. Kulia ni Mtafiti kutoka TALIRI, Neema Urassa na wa pili kulia (aliyevaa kofia ya njano) ni Mkurugenzi wa TALIRI Kanda ya Mashariki, Dkt. Zabron Nziku.



Makatibu Wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi wakisalimiana punde walipokutana leo Julai 5, 2020 katika Maonesho ya Kimataifa ya 44 ya biashara (Sabasaba) yanayofanyika katika Uwanja wa Mwl. Nyerere, Barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi(Mifugo), Prof. Elisante Ole Gabriel na Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi), Dkt. Rashid Tamatama.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Elisante Ole Gabriel(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Kampuni ya AKM Glitters inayofanya shughuli zake jijini Dar es Salaam. Prof. Gabriel alitembelea Kampuni hiyo mapema leo Julai 5, 2020 kwa lengo la kuona shughuli wanazofanya. Kampuni hiyo inajishughulisha na ufugaji wa kuku aina ya Kuroiler, Kutotolesha Vifaranga na Kusaga vyakula vya kuku.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni