Nav bar

Jumatano, 3 Aprili 2019


SERIKALI YATEKETEZA TANI 8 ZA NYAMA ZILIZOKWISHA MUDA WA MATUMIZI.

Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeteketeza tani 8 za nyama kutoka maeneo mbalimbali mkoani Arusha ambazo zimebainika zimekwisha muda wake wa matumizi na hazifai kwa matumizi ya binadamu.

Tukio hilo la uteketezaji wa nyama limefanyika tarehe (22.03.2019) eneo la Njiro likiongozwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Luhaga Joelson Mpina (Mb) ambapo tani hizo za nyama zilikamatwa wakati wa Operesheni Nzagamba II Viwandani.

Kufuatia tukio hilo la uteketezaji wa bidhaa za mifugo na mazao yake, Waziri Mpina alisema hatuta endelea kuangalia uozo ukiendelea kufanyika na tutahakikisha tunaendelea kudhibiti uiongizaji holela wa mazao hayo na zilizokwisha muda wake wa matumizi.

“Operesheni yetu hii ni ya kila siku na tunaendelea kutokomeza mazao ya mifugo yanayoingia nchini bila vibali hatutafikia mwisho mpaka jambo hili likamilike, alisema Waziri Mpina”.


Waziri Mpina alisema, hakuna mtu atakayewekeza kwenye nchi yetu kama hatuwezi kusimamia vizuri masoko yetu ya ndani na kuwalinda wenye viwanda vyetu.


“Ukiruhusu taifa likaenda namna hii ni nani mwekezaji wa nchi yeyote atakayekuja kuwekeza kwenye nchi ambayo inaruhusu mtu kuingiza bidhaa bila utaratibu,  alisemaWaziri Mpina

Waziri Mpina alisema, rasilimali za nchi lazima wananchi wanufaike nazo, mifugo haiwezi kuchukuliwa na mtu yeyote  ikavushwa na kutumika na watu wengine bila sisi kulipia ushuru kwa mujibu wa sheria.

“Lazima wananchi, wawekezaji na wafanyabiashara wote wafuate sheria na taratibu mbalimbali za nchi yetu zinazozuia kuingiza bidhaa ambazo hazijathibitishwa ubora wake na kukaguliwa”. alisema Waziri Mpina

Serikali haitachoka kuendelea kuchukua hatua kali na watendaji wa serikali lazima mhakikishe mnakua makini maeneo yote ya mipaka yetu, na kuteketeza huku kunaniuma lakini hatuwezi kuacha kuendeleza uovu uendelee kutokea operesheni na doria hizi hazitafika mwisho hadi hapo hali itakapokuwa imerejea, alisisitiza Waziri Mpina.

Nikiwa kama Waziri mwenye dhamana ya Wizara yangu ya mifugo na uvuvi ningependa watu wanaofanya biashara ya mifugo na mazao yake wanufaike na watajirike, alisisitiza Waziri Mpina.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Arusha Bw. Mrisho Gambo amesema wamegundua Waziri Mpina amefanya mambo mengi na kuna vitu vizuri ambavyo wizara imefanya kwa maslahi ya ndani ya nchi. 

“Serikali ya Mkoa wa Arusha tunakuunga mkono na tupo bega kwa bega kushirikiana na wale ambao hawataki kufuata sheria na maslahi ya nchi na tunashukuru waziri umejiridhisha na mzigo huo umeonekana na kufukuliwa, watu waache tabia ya kujichukulia sheria mkononi, alisema Bw. Gambo


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni