TAHARIFA KWA UMMA KUHUSU TAHADHARI YA MLIPUKO WA UGONJWA WA HOMA WA BONDE LA UFA (RVF)
Ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (RVF) ni ugonjwa hatari kwa binadamu na mifugo hususan ng’ombe, mbuzi, kondoo na ngamia ambao husababishwa na virusi jamii ya Bunyaviridae . Wanyama huambukizwa kwa kuumwa na mbu aina ya ‘Aedes”. Binadamu hupata ugonjwa kwa kushika au kula nyama ya mnyama aliyeambukizwa na virusi vya ugonjwa huo Katika siku za hivi Mamlaka ya Hali ya Hewa Kenya, Shirika la Afya ya Wanyama Duniani (OIE) na Shirika la Afya Duniani (WHO) wametoa taarifa za matukio ya ugonjwa wa Homa ya Bonde la Ufa (RVF) Kaskazini mwa Kenya na Mashariki mwa nchi ya Rwanda. Hata hivyo Ugonjwa huo haupo hapa nchini. Kutokana na kuwepo kwa ugonjwa huu katika nchi jirani, Wizara inatoa maelekezo yafuatayo kwa Halmashauri zote nchini (Idara za Mifugo, Afya na Elimu) na mikoa yote kuzingatia yafuatayo ili kuchukua tahadhari zote zinazotakiwa ili ugonjwa huu usiweze kuingia nchini. (a) Halmashauri zianze kutoa taarifa n...