KAMATI YA BUNGE YARIDHIA UPUMZISHWAJI WA SHUGHULI ZA UVUVI ZIWA TANGANYIKA
Na Hamis Hussein, MLF Dodoma. Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeridhia Upumzishwaji wa shughuli za uvuvi kwa ziwa Tanganyika uendelee kulingana na manufaa yanayopatikana kutokana na takwimu zinavyoeleza. Akizungumza wakati wa Semina kuhusu upumzishwaji wa shughuli wa Ziwa Tanganyika kwa mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi uliopo Bungeni jijini Dodoma Machi 28, 2025 Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Deodatus Mwanyika amesema wizara iendelee kufanya utafiti katika ukanda wote wa ziwa Tanganyika ili kubaini changamoto na kuzitatua. Aidha Mhe. Mwanyika ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuendele kulinda rasilimali za Taifa kwa manufaa ya Wananchi wake, vilevile amesisitiza kuwa udhibiti wa uvuvi haramu lishughulikiwe kwa nguvu kubwa. Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameielekeza kikosi cha kuzuia uvuvi Haramu kuelekea ziwa Tanganyika na kuondoa Nyavu zote zinazotumika kwenye uvuvi Haramu (Gi...