Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2025

KAMATI YA BUNGE YARIDHIA UPUMZISHWAJI WA SHUGHULI ZA UVUVI ZIWA TANGANYIKA

Picha
Na Hamis Hussein, MLF Dodoma. Kamati ya kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo imeridhia Upumzishwaji wa shughuli za uvuvi kwa ziwa Tanganyika uendelee kulingana na manufaa yanayopatikana kutokana na takwimu zinavyoeleza. Akizungumza wakati wa Semina kuhusu upumzishwaji wa shughuli wa Ziwa Tanganyika kwa mwaka 2025 iliyofanyika katika ukumbi uliopo Bungeni jijini Dodoma Machi 28, 2025  Mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe.  Deodatus Mwanyika amesema wizara iendelee kufanya utafiti katika ukanda wote wa ziwa Tanganyika ili kubaini changamoto na kuzitatua. Aidha Mhe. Mwanyika ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kuendele kulinda rasilimali za Taifa kwa manufaa ya Wananchi wake, vilevile amesisitiza kuwa udhibiti wa uvuvi haramu lishughulikiwe kwa nguvu kubwa. Kwa upande wake Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameielekeza kikosi cha kuzuia uvuvi Haramu kuelekea ziwa Tanganyika na kuondoa Nyavu zote zinazotumika kwenye uvuvi Haramu (Gi...

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI 2024/2025

Picha
Na Hamis Hussein, MLF Dodoma. ⬛️ Yaahidi Kuisemea Wizaya hiyo kuongezewa Fedha Kamati ya Kudumu ya Viwanda,Biashara, Kilimo na Mifugo, chini ya Kaimu Mwenyekiti wake Mhe. Dkt. Medadi Kalemani Machi 27, 2025 imepokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya  Mifugo na Uvuvi katika mwaka wa fedha 2024- 2025 na kuridhia mpango na bajeti ya mwaka fedha 2025- 2026. Akizungumza kwenye kikao hicho Kaimu Mwenyekiti wa Kamati Mhe. Dkt. Medadi Kalemani ameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi ambayo licha ya kuwa na bajeti ndogo lakini imeweza kutekeleza miradi ya kimkakati. " Wizara hii  huwa haipati bajeti kubwa sana ukilinganisha na Wizara zingine lakini imeweza kutekeleza miradi ya kimkakati ambayo inaenda kuleta tija kwa wananchi, hivyo Mhe. Waziri na watumishi wote wa Wizara sisi kamati tutaendelea kuishauri serikali ili iongeze bajeti kwenye sekta hii ya mifugo na uvuvi kwani inatoa utajiri kwa wananchi, lakini pia mtuombee na sisi turudi ili tuendelee kuwasemea...

DKT. KIJAJI AWATAKA WATUMISHI WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI KUWA WAZALENDO

Picha
Na. Stanley Brayton ◼️Ataka watumishi kuwatumikia vyema wananchi Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, amewataka watumishi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kuwa na utumishi wa kizalendo uliotukuka kwa Watanzania ili kuweza kusongambele katika Sekta hizo mbili. Akizungumza na watumishi wa Wizara hiyo leo Machi 26, 2025 katika Kikao chake na watumishi hao, kilicho jumuisha Wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi za Wizara, kilichofanyika katika Ofisi za Makao Makuu ya Wizara katika Mji wa Kiserikali Mtumba, Dkt. Kijaji amesema anafurahishwa sana na utendaji mzuri wa watumishi wa Wizara hiyo huku akiwapongeza kwa kazi nzuri wanazozifanya katika kuendeleza sekta za mifugo na uvuvi. "wizara inaonekana jinsi inavyofanya kazi  na inaendelea kufanya kazi vyema kwani tangu tuanze kuzunguka na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, tulikopita kwenye Miradi yetu yote walitupongeza na kusema tumefanya vizuri" amesema Dkt. Kijaji. Aidha, Dkt. Kijaji amemshuk...

SERIKALI YATAMBULISHA MRADI MPYA WA KIMAGEUZI KATIKA TASNIA YA MAZIWA

Picha
Na. Stanley Brayton Serikali imeendelea kufanya juhudi za kuimarisha na kuweka mikakati  bora ya kukuza Tasnia ya Maziwa kwa kutambulisha Mradi mpya wa Kimageuzi  wa Tasnia hiyo. Akizungumza katika  Warsha hiyo ya  kutambulisha  Mradi wa Kimageuzi wa Tasnia ya Maziwa iliyofanyika leo Machi 17, 2025 mkoani Dodoma katika Ukumbi  wa Hoteli ya Rafiki, Katibu Mkuu Wizara  ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe, amesema Mradi huu utagharimu kiasi cha Dola 174.36 za Kimarekani na ni muhimu sana kwa watanzania wengi. "tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kuwepo kwa Mradi huu ambao utasaidia kunyanyua uchumi wa Watanzania na nchi kiujumla" amesema Prof. Shemdoe  Aidha, Prof. Shemdoe ameelekeza kuwa Mradi huo uzingatie thamani ya fedha, muda pamoja na matokeo  chanya yanayolenga kuwanufaisha vijana, wakina mama pamoja na makundi maalum  Vilevile, Prof. Shemdoe ameeleza kuwa Mradi h...