Nav bar

Alhamisi, 14 Septemba 2023

PROF. SHEMDOE ASISITIZA MAMBO SITA YA KUZINGAZIA KATIKA UANDAAJI WA MRADI WA MAZIWA

Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe leo tarehe 13 Sept 2023, ameshiriki ufunguzi wa mkutano unaoandaa andiko la mradi wa kuongeza uzalishaji wa maziwa huko Kigali nchini Rwanda kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi, na kupunguza gesi joto kwa nchi nne za Africa Mashariki (Kenya, Rwanda, Tanzania, na Uganda)

Aidha, Mkutano huo wa siku tatu unaofanyika nchini humo, Prof.Shemdoe amewaelekeza washiriki kufikiria kuelekeza fedha  na utaalam wa mradi huo kwa Upande wa Tanzania katika maeneo sita ambayo ni pamoja na BBT-LIFE, kuongeza ushiriki wa vijana na wanawake, kuongeza utajiri kwa wadau, kuongeza uzalishaji, kuimarisha mradi wa kopa ng'ombe lipa maziwa  na kutilia mkazo suala la  "Livestock Guest House".


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe leo tarehe 13.09.2023 akifuatilia kwa makini Mkutano wa uandaaji wa andiko la mradi wa kuongeza uzalishaji wa maziwa kwa kuzingatia mabadiliko ya tabia nchi na kupunguza gesi joto kwa nchi  za Africa Mashariki.


Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe (Kushoto) akiteta jambo leo tarehe 13/09/2023, na Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na rasilimali za Mifugo wa Rwanda Dr. Olivia Kamana ambapo pia wamekubaliana kuwa na mpango wa pamoja wa chanjo ya Mifugo.



Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof.Riziki Shemdoe, leo tarehe 13 Sept 2023 akizungumza akiwa Kigali nchini Rwanda wakati wa ufunguzi wa mkutano wa siku tatu wa Uandaaji wa andiko la mradi wa kuongeza Uzalishaji wa Maziwa kwa kuzingatia madiliko ya tabia nchi na kupunguza gesi joto kwa nchi za Africa Mashariki.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni