Nav bar

Alhamisi, 14 Septemba 2023

FAO KUTOA MSAADA WA KOMPYUTA KWA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI

Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina akiongea na wawakilishi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo duniani (FAO) (Hawapo pichani) walipowasili kwenye ofisi za Wizara hiyo zilizopo mtumba jijini Dodoma lengo likiwa ni pamoja na kukabidhi kompyuta zilizoombwa kwa ajili ya kusaidia kwenye kituo cha huduma kwa wateja kinachitarajiwa kuanzishwa Wizarani hapo   , Septemba 12,2023


Mshauri Mwelekezi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani  (FAO) Bw. Monday Ahonsi akieleza lengo la shirika hilo kutoa msaada wa compyuta kwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikiwa ni pamoja na kusaidia kwenye shughuli za kituo cha huduma kwa wateja kinachotarajiwa kianzishwa wizarani hapo, Septemba 12,2023  jijini Dodoma.


Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia ya habari na Mawasiliano (TEHAMA) Bw. Baltazari Kibola (kulia) akichangia hoja wakati wa kikao kifupi na wawakilishi kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) kilichofanyika kwenye ofisi za Wizara ya Mifugo na Uvuvi mtumba jijini Dodoma , Septemba 12, 2023


Kaimu Katibu Mkuu kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina (kushoto) akipokea msaada wa kompyuta zitakazosaidia kwenye kituo cha huduma kwa wateja kinachotarajiwa kuanzishwa kwenye Wizara hiyo kutoka kwa Mshauri Mwelekezi wa  Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO). Bw. Monday  Ahonsi (wa pili kutoka kulia) mara baada ya kikao kifupi kilichofanyika  mtumba jijini Dodoma, Septemba 12,2023.



 Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina (wa nne kutoka kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na watendaji kutoka Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na watendaji wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi mara baada ya kupokea msaada wa  kompyuta kutoka FAO, Septemba 12, 2023 jijini Dodoma.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni