Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2020

TUTAHAKIKISHA WAFUGAJI WOTE WANAFUGA KISASA NA KWA TIJA- DKT. MRUTTU

Picha
Kaimu Mkurugenzi wa Utafiti na Mafunzo, Dkt. Hassan Ally Mruttu  amewataka wafugaji mkoani Pwani  kufuga kisasa na kwa tija huku wakichukua tahadhari dhidi ya maambukizi ya virusi vya korona.  Akiongea wakati wa Mafunzo elekezi na uhamasishaji  kwa ajili ya kupandisha ng'ombe kwa njia ya chupa (uhimilishaji) kwenye kijiji cha Mkwalia kitumbo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga jana ( 22/04/2020) Dkt. Mruttu amesema lengo la Mafunzo hayo ni kutaka wafugaji kufuga kisasa na kupata Mifugo iliyo bora na mizuri ili kuwezesha wafugaji kufaidika na Mifugo yao. "Ni jukumu la Wizara  kuhakikisha wafugaji wote nchini wanapata mbegu bora kwa njia ya uhimilishaji ili kupata Mifugo iliyo bora." Alisema Dr. Mrutu. Aidha ametoa wito kwa wataalam wa Mifugo kuwa tayari wakati wowote kuwasaidia wafugaji pindi wanapotaka kupandikiziwa mbegu bora kwenye Mifugo yao. Naye Mtafiti wa Mifugo, Bi. Neema Urassa kutoka taasisi ya utafiti wa Mifugo nchini (TALIRI...

"NARCO ijiandae kuwa kitovu cha kuuza mifugo na bidhaa zake baada ya CORONA" Prof. Ole Gabriel

Picha
 Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel ameitaka hifadhi ya ranchi za taifa (NARCO) kwa kushirikiana wadau wengine wa sekta ya Mifugo kuhakikisha Nchi inakuwa na Mifugo ya kutosha na yenye afya kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya bidhaa zitokanazo na mifugo wakati huu wa janga la Ugonjwa wa homa kali ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona (Covid 19) na hata mara baada ya janga hilo kuisha. Prof. Elisante Ole Gabriel aliyasema hayo mapema leo (18.04 2020) mchana alipofanya ziara katika Wilaya ya Muleba mkoani Kagera lengo likiwa ni kukagua utekelezaji marekebisho ya upimaji wa ramani ya Ranchi ya Mwisa II ili kutenga eneo lililopendekezwa  kuhamishia wananchi waishio ndani ya Ranchi hiyo. "Wakati huu wa hili janga la Corona mahitaji ya nyama Afrika na duniani ni makubwa sana na yanaweza kuongezeka maradufu mara baada ya janga hili kuisha hivyo ni lazima tujipange ili kuhakikisha tunakuwa kitovu cha usambazaji wa bi...