SERIKALI YAENDELEA KUTOA MAFUNZO YA UPANDIKIZAJI VIFARANGA VYA SAMAKI KWENYE VIZIMBA NA MABWAWA
Na. Stanley Brayton, MWUV ◾ Vifaranga 1,500 vya pandikizwa Viwanja vya Maonesho Nanenane Dodoma. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imeendelea kutoa Mafunzo ya Upandikizaji Vifaranga vya Samaki ili kuwafanya wadau wa Sekta hiyo kuwa na Ujuzi wa kutosha katika kufuga Samaki pamoja na kuwasaidia kuwapa mbinu bora na ya kisasa ya ufugaji Samaki ili kuweza kujipatia kipato na lishe. Akizungumza katika zoezi hilo la Upandikizaji wa Vifaranga vya Samaki katika Viwanja vya Maonesho ya Nanenane ya Dkt. John Samwel Malecela, leo Oktoba 28, 2025 jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Viumbe Maji Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Nazael Madalla amesema lengo kubwa la kupandikiza Samaki katika Vizimba na Mabwawa yaliopo katika Viwanja vya Maonesho ya nanenane ni kuwawezesha wadau wa Sekta kupata Mafunzo ya teknolojia mpya ya ufugaji wa Samaki kwa njia ya Vizimba pamoja na Mabwawa. "Wizara inaendelea kuhamisha, kuendeleza pamoja na kusimamia shughuli za Ukuzaji Viumbe Maji kwa kut...