Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Aprili, 2025

SERIKALI KUENDELEA KUWEZESHA UFUGAJI WA KISASA

Picha
Na Hamisi Hussein - WMUV, Mwanza. ⬛️ Mhe. Mnyeti akikabidhi Mitamba 10 ya Maziwa kwa UWAMATA Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kuwezesha ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija katika uzalishaji na kukuza uchumi wa wafugaji nchini. Hayo yameelezwa leo Aprili 19, 2025 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alaxender Mnyeti wakati wa kukabidhi ng'ombe 10 wa Maziwa kwa kikundi cha Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) hafla iliyofanyika katika Shamba la Uzalishaji Mifugo lililopo Misungwi mkoani Mwanza. Mhe. Mnyeti amesema lengo la serikali nikuona inawezesha ufugaji wa kisasa kwa kuhimiza wafugaji kuwa na mifugo michache yenye tija itakayotoa mazao bora yanayokidhi  ushindani wa masoko. " Mhe. Rais wetu anataka kuona ufugaji wa Kisasa unakuwa na tija kwa wafugaji na sisi Wizara tunaendelea kuhimiza ufugaji wa kisasa ambapo tumekuwa tukihamasisha ulimaji wa malish...

TDB YAHIMIZWA KUENDELEA KUSAJILI WADAU WA TASNIA YA MAZIWA

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV  Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte ameihimiza Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) kuendelea kuwatambua na kuwasajili wadau wa Tasnia ya Maziwa ili kuongeza Uzalishaji wa maziwa nchini. Ndg. Mhinte amesema hayo wakati akizungumza na Watumishi wa TDB katika Kikao kazi kinachofanyika kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Aprili 16, 2025. "kama wadau wa Tasnia ya Maziwa hawafahamiki na hawajasajiliwa, ni ngumu sana kufikia Malengo na kuzalisha Maziwa kwa wingi, kwani wanahitaji kutatuliwa changamoto zao, ikiwemo za Masoko ya Maziwa hayo" amesema Ndg. Mhinte  Vilevile, Ndg. Mhinte amesema kuwa wadau wa Tasnia ya Maziwa wapo sehemu mbalimbali nchini, na ni vyema Vituo vya ukusanyaji Maziwa vikarekebishwa na kuongezwa, ikiwa pamoja na Usimamizi  mzuri ili Maziwa yakusanywe kwa wingi. Ndg. Mhinte, pia amehimiza Bodi kubuni Miradi mbalimbali kama ya Bar za Maziwa ili kuhakikisha Watumishi wanayapata kiurahisi na kuongeza P...

​KONGAMANO LA KITAIFA LA NGURUWE KUFANYIKA TANZANIA

Picha
Na. Chiku Makwai (MUV). Dodoma Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi ikishirikiana na chama cha wafugaji wa Nguruwe Tanzania (TAPIFA) imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa kongamano la kimataifa la ufugaji wa nguruwe litakalo fanyika Septemba 11-13, 2025 jijini Dar es Salaam. Hayo yamesemwa leo Aprili 16, 2025 na Naibu Waziri, Wizara ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Alexander Mnyeti Wakati wa Mkutano na Waandishi wa Habari Uliofanyika katika Ukumbi uliopo jengo la NBC jijini Dodoma. Mhe. Mnyeti amesema kuwa kongamano hilo linatarajiwa kuhudhuriwa na washiriki takribani 2000 kutoka mataifa mbalimbali barani Afrika wakiwemo Viongozi wa Serikali na Wizara za kisekta, Wawekezaji wa ndani na nje ya nchi, Vijana na Wanawake, Wanataaluma, Wadau wa Maendeleo, Wafugaji na Wafanyabiashara katika mnyororo wa thamani wa Nguruwe. Aidha, ameongeza kuwa kongamano hilo litaambatana na Mafunzo kutoka kwa wataalam na Wadau wa Maendeleo katika tasnia ya Nguruwe, pia washiriki kufanya majadiliano ya kibiashara na...

WAFUGAJI WAHIMIZWA KUPANDA MALISHO YA MIFUGO

Picha
Na. Stanley Brayton, WMUV - Dodoma ◼️Waelezewa athari za kulisha Mifugo katika maeneo ya Hifadhi za Misitu. Naibu Katibu Mkuu Wizara  ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, amewataka wafugaji Wilayani Bahi na Chamwino kupanda Malisho kwa ajili ya Mifugo ili kuepukana na changamoto za kukosa Malisho ya Mifugo. Akizungumza katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika leo Aprili 15, 2025, Mkoani Dodoma, katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Wilaya ni Bahi, Ndg. Mhinte, amesema yapo maeneo muhimu ya Malisho ambayo yametengwa na Serikali ili kutatua changamoto za Malisho. "yapo maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya Malisho japo yanapungua kadri Mifugo inavyozidi kuongezeka, na ni muhimu kuhakikisha kila mfugaji anapanda Malisho kwa ajili ya Mifugo yake" amesema Ndg. Mhite  Vilevile, Ndg. Mhite amebainisha kuwa maeneo ya Malisho yanapungua kadri Mifugo na watu wanavyoongezeka, kiasi cha kwamba kun...

DKT. MHINA AWATAKA WATUMISHI KUZINGATIA WELEDI, UAMINIFU NA WAJIBU

Picha
Na. Chiku Makwai (WMUV). Dodoma Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali Watu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt. Charles Mhina amewataka watumishi wa Bodi ya Maziwa Tanzania (TDB) kuzingatia weledi, uaminifu na wajibu katika kutekeleza majukumu yao. Ameyasema hayo Aprili 15, 2025 wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha  menejimenti pamoja na watumishi wa bodi hiyo kilichofanyika katika moja ya ukumbi ziliopo katika Ofisi ya Mkuu wa Dodoma.  Aidha,  Dkt Mhina ameipongeza TDB kwa kuendelea kupiga hatua katika utoaji huduma zilizo bora na amewasisitiza kuwa ili kupata maendeleo ni wajibu wa kila mtumishi kufanya kazi kwa bidii.  Kwa upande wake Msajili Mkuu wa TDB Prof. George Msalya amesema kuwa Tasnia ya Maziwa inazidi kukua nchini na mpaka sasa kuna zaidi ya viwanda 152 vya uchakataji maziwa. Vile vile ameongeza kuwa ipo mipango mbalimbali inayoandaliwa na kuratibiwa na bodi hiyo itakayolenga kuhamasisha unywaji maziwa nchini pamoja na manufaa yake. Mkurugenzi wa Ida...

SHEMDOE ABAINISHA FURSA ZA MALISHO YA MIFUGO

Picha
Na. Omary Mtamike Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Riziki Shemdoe amewataka wafugaji nchini kuendelea kutenga maeneo ya kuzalisha malisho ya mifugo yao ili waendelee kuboresha afya za wanyama na kujipatia kipato baada ya kuyauza. Prof. Shemdoe amesema hayo Aprili 14,2025 wakati akifungua kikao cha wataalam wa malisho ya Mifugo kilichofanyika mkoani Morogoro ambapo ametoa rai kwa vijana kuchangamkia fursa hiyo kama wanavyofanya kwenye shughuli nyingine za kiuchumi. “Tuwawezeshe vijana waanzishe mashamba ya kulima malisho kwa sababu nina uhakika masoko yapo na nina mfano wa mtu mmoja hapa Pwani yeye kila mwaka anauza tani nyingi za malisho na hana biashara nyingine zaidi ya hiyo” Ameongeza Prof. Shemdoe. Aidha katika hatua ya utekelezaji wa maazimio ya kikao kilichopita cha wataalam hao, Prof. Shemdoe amesema Wizara yake imeendelea kuajiri vijana wengi wanaotokana na shahada ya nyanda za malisho huku pia wakiendelea kutoa elimu kuhusu chakula stahiki kwa mifugo. Akizungumza...

NDEGE NYUKI YAANZA RASMI KUWASAKA WAVUVI HARAMU ZIWA VICTORIA

Picha
Na Edward Kondela - WMUV, Mwanza Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa mara ya kwanza imenunua na kuzindua matumizi ya ndege nyuki (drone) itakayofanya kazi ya kuimarisha usimamizi wa shughuli za uvuvi katika Ziwa Victoria. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ndege nyuki hiyo jijini Mwanza Aprili 13, 2025 kwa niaba ya Mgeni Rasmi Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji, Naibu Waziri wa wizara hiyo Mhe. Alexander Mnyeti amesema serikali imeamua kuchukua hatua madhubuti za kisasa kuhakikisha inadhibiti uvuvi haramu kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Mhe. Mnyeti ameongeza kuwa katika awamu hii wizara imetumia kiasi cha Shilingi Milioni 259, kwa ajili ya ununuzi wa ndege nyuki, kutoa mafunzo kwa waendeshaji, kufunga vituo vya kudhibiti, kufanya usajili na kuanzisha mfumo wa kuhifadhi na kuchambua taarifa zinazopatikana kutoka kwenye ndege hiyo. “Ndege nyuki hii ni kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa shughuli za uvuvi katika Ziwa Victoria. Ndege nyuki hii ina uwezo wa kukim...

MIFUGO ZAIDI YA MILIONI 370 IMEPATIWA CHANJO DHIDI YA MAGONJWA

Picha
Na. Chiku Makwai - MUV, Dodoma. Serikali kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imetoa chanjo kwa mifugo zaidi ya milioni 370 kwa lengo la kutibu na kuzuia magonjwa aina ya kiimeta na homa ya mapafu, pamoja na  mifugo kukidhi matakwa ya soko la kimataifa.  Hayo yameelezwa leo (Aprili 9, 2025) na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa wakati akitoa hotuba kuhusu Mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali na Makadirio na Mapato na Matumizi ya Fedha za Ofisi ya Waziri Mkuu na Ofisi ya Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 bungeni jijini Dodoma.  “Kwa kuimarisha huduma za ugani na kudhibiti magonjwa ya mifugo yanayovuka mipaka, katika kipindi cha Mwezi Julai, 2024 hadi Mwezi Januari 2025, serikali imenunua chanjo zenye thamani ya Shilingi Bilioni 10.1 kwa ajili ya kudhibiti magonjwa ya mifugo nchin.i” amesema Mhe. Waziri Mkuu Aidha Mhe. Waziri Mkuu amesema kuwa kwa kutambua umuhimu wa ufugaji wa kisasa unaozingatia malisho bora na idadi ya mifugo inayoweza k...

WATUMISHI WA LITA WAHIMIZWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA

Picha
Na. Stanley Brayton ◼️Ataka watumishi kufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina amewataka watumishi wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) kuzingatia Kanuni za Maadili ya Utumishi wa umma kwani taasisi yeyote ambayo haizingatii maadili ya Utumishi wa Umma ni vigumu sana kupata utendaji wenye tija. Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe leo Aprili 04, 2025 Dodoma katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Mhina amesema kuna baadhi ya Watumishi wanashindwa kuzingatia Kanuni za maadili na Sheria za utumishi wa umma kutokana na uzembe na matokeo yake kuleta matokeo mabovu katika Taasisi. "Tufanye kazi kwa bidii na kwa uaminifu kazini kwa kufuata misingi Mikuu ya Uadilifu, ikiwemo uwajibikaji na uaminifu," amesem...