SERIKALI KUENDELEA KUWEZESHA UFUGAJI WA KISASA
Na Hamisi Hussein - WMUV, Mwanza. ⬛️ Mhe. Mnyeti akikabidhi Mitamba 10 ya Maziwa kwa UWAMATA Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi itaendelea kuwezesha ufugaji wa kisasa ili kuongeza tija katika uzalishaji na kukuza uchumi wa wafugaji nchini. Hayo yameelezwa leo Aprili 19, 2025 na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Alaxender Mnyeti wakati wa kukabidhi ng'ombe 10 wa Maziwa kwa kikundi cha Umoja wa Mapadri Tanzania (UWAMATA) hafla iliyofanyika katika Shamba la Uzalishaji Mifugo lililopo Misungwi mkoani Mwanza. Mhe. Mnyeti amesema lengo la serikali nikuona inawezesha ufugaji wa kisasa kwa kuhimiza wafugaji kuwa na mifugo michache yenye tija itakayotoa mazao bora yanayokidhi ushindani wa masoko. " Mhe. Rais wetu anataka kuona ufugaji wa Kisasa unakuwa na tija kwa wafugaji na sisi Wizara tunaendelea kuhimiza ufugaji wa kisasa ambapo tumekuwa tukihamasisha ulimaji wa malish...