Na. Stanley Brayton, WMUV - Dodoma
◼️Waelezewa athari za kulisha Mifugo katika maeneo ya Hifadhi za Misitu.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, amewataka wafugaji Wilayani Bahi na Chamwino kupanda Malisho kwa ajili ya Mifugo ili kuepukana na changamoto za kukosa Malisho ya Mifugo.
Akizungumza katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika leo Aprili 15, 2025, Mkoani Dodoma, katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Wilaya ni Bahi, Ndg. Mhinte, amesema yapo maeneo muhimu ya Malisho ambayo yametengwa na Serikali ili kutatua changamoto za Malisho.
"yapo maeneo ambayo yametengwa kwa ajili ya Malisho japo yanapungua kadri Mifugo inavyozidi kuongezeka, na ni muhimu kuhakikisha kila mfugaji anapanda Malisho kwa ajili ya Mifugo yake" amesema Ndg. Mhite
Vilevile, Ndg. Mhite amebainisha kuwa maeneo ya Malisho yanapungua kadri Mifugo na watu wanavyoongezeka, kiasi cha kwamba kunapelekea Misitu na Malisho kupungua au kutoweka kabisa.
Pia, Ndg. Mhinte ametolea ufafanuzi kuhusu athari za kulisha Mifugo katika maeneo ya Hifadhi ya Misitu, ikiwa ni pamoja na kuharibu Hifadhi hiyo na hatimaye kuamia katika Hifadhi zingine na kuziharibu na mwishowe kukosa Malisho kabisa pamoja na kuharibu Hifadhi hizo.
Ndg. Mhinte amesema kuwa Biashara ya kupanda Malisho imekuwa kama Dhahabu na hii ndio itakayosaidia wafugaji wengi katika kulisha Mifugo yao.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za vyakula za Mifugo. Dkt. Asimwe Rwiguza, amesema kwa sasa Serikali haitegemei Malisho ya asili kwa sababu haitoshelezi idadi ya Mifugo ambayo tunayo hapa nchini.
Dkt. Rwiguza amefafanua kuwa kwa sasa kuna namna ya kukabiliana na changamoto za Malisho, ikiwa ni pamoja na kulima Malisho, na ndio maana Serikali imetoa maeneo maalum kwa ajili ya kupanda Malisho na inaendelea kutoa mbegu hizo za Malisho na kutoa elimu namna ya kupanda hizo mbegu ili kuhakikisha kila mfugaji anakuwa nazo na anapandikiza katika eneo lake.
Akizungumza kwa niaba ya wafugaji wote, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT), Bw. Kusundwa Wamalwa amesema zipo changamoto nyingi zinazowakumba wafugaji wengi hususan wa hapa Wilaya ya Bahi na Chamwino, ikiwemo Maji, Malisho na Masoko, kwa hiyo ni vyema Serikali ikaangalia ni jinsi gani itaweza kutatua changamoto zinazowakabili wafugaji hao
Naye, Kamanda wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kati ambaye ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Bw. Mathew Kiondo amesema miaka ya nyuma TFS ilitoa Hekta 2000 kwa wafugaji, ila kutokana na ongezeko la watu limepelekea Mahitaji ya Malisho kuwa makubwa kutokana na idadi kubwa ya watu na Mifugo, kwa hiyo wao kama TFS wataangalia ni jinsi gani wataweza kufanya ili kunasua wafugaji na changamoto ya uhaba wa maji kupitia Mfuko wa Kusaidia Jamii (CSR), ili kuwatengenezea Miundombinu ya maji kutoka kwenye Hifadhi ya Msitu wa Chenene kwenda kwenye maeneo yao ya Ufugaji.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte, akizungumza na Wafugaji wa Wilaya ya Chamwino na Bahi katika kikao chake na Wafugaji hao cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Wilayani Bahi, Dodoma, Aprili 15, 2025.
Katibu Tawala Msaidizi - Sekta za Uchumi Mkoa wa Dodoma, Bi. Aziza Mumba, akizungumza na Wafugaji na kuelezea umuhimu wa Sekta ya Mifugo katika kuchangia Pato la Taifa, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
MKurugenzi wa Idara ya Uendelezaji wa Maeneo ya Malisho na Rasilimali za vyakula za Mifugo. Dkt. Asimwe Rwiguza, akitoa ufafanuzi kwa wafugaji juu ya umuhimu wa kupanda na Malisho kwa ajili ya Mifugo ili kutatua changamoto zao, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Wafugaji Tanzania (CCWT), Bw. Kusundwa Wamalwa, akimuelezea Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), changamoto wanazokumbana nazo wafugaji nchi ikiwemo Maji, Malisho na Masoko, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Kamanda wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Kati ambaye ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Bw. Mathew Kiondo, akiwaelezea wafugaji umuhimu wa Hifadhi ya Msitu wa Chenene Mashariki na Magharibi ambao umeingia kwenye Halmashauri zote mbili za Bahi na Chamwino na kubainisha jinsi watakavyozitatua changamoto za wafugaji katika Malisho na maji, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Mfugaji, Bw. Anthony Makaka, akiiomba Serikali kuweka utaratibu wa kupata Malisho ili kutatua changamoto zao ikiwa pamoja na kuwapatia mabwawa kwa ajili ya Mifugo na matumizi yao binafsi, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Mfugaji, Bw. Manimba oloya, akielekeza jinsi Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wanavyokamata Mifugo yao wakati wanapoipeleka kwenye Malisho katika Hifadhi ya Msitu wa Chenene kutokana na kutoandaliwa sehemu za Malisho na kuwapatia elimu ya kutosha, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Mfugaji, Bi. Kafutuku Kipara, akielezea changamoto alizokutana nazo za kuchukuliwa maeneo yake ya kufugia, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Mfugaji, Bi. Katarina Garabuu, akielezea changamoto anazokumbana nazo akienda katika Hifadhi ya Msitu wa Chenene katika kutafuta Maji kwa ajili ya Mifugo, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Mfugaji, Bw. Tadayo Sembuche, akilalamikia faini kubwa wanazotozwa na kunyang'anywa Mifugo baada ya kuingia Mifugo hiyo katika Hifadhi ya Msitu wa Chenene, katika Kikao na Wafugaji cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika katika Kitongoji Cha Mtungutu, Kata ya Zanka, Kijiji Cha Mayamaya, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Picha ni baadhi ya wafugaji, wakimsikiliza Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte (hayupo pichani), akielezea kuhusu, katika Kikao chake na Wafugaji hao cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika Mtungutu Kijiji cha Mayamaya kata ya Zanka, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo), Ndg. Abdul Mhinte (waliokaa katikati), akiwa kwenye picha ya pamoja na Wafugaji wa Wilaya ya Chamwino na Bahi, baada ya Kikao chake na Wafugaji hao cha kujadili changamoto zao na kuzitafutia Ufumbuzi, kilichofanyika Mtungutu Kijiji cha Mayamaya kata ya Zanka, Aprili 15, 2025, Bahi - Dodoma.