Nav bar

Ijumaa, 4 Aprili 2025

WATUMISHI WA LITA WAHIMIZWA KUZINGATIA MAADILI YA UTUMISHI WA UMMA

Na. Stanley Brayton

◼️Ataka watumishi kufanya kazi kwa bidii na kwa uaminifu

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina amewataka watumishi wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) kuzingatia Kanuni za Maadili ya Utumishi wa umma kwani taasisi yeyote ambayo haizingatii maadili ya Utumishi wa Umma ni vigumu sana kupata utendaji wenye tija.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Riziki Shemdoe leo Aprili 04, 2025 Dodoma katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Mhina amesema kuna baadhi ya Watumishi wanashindwa kuzingatia Kanuni za maadili na Sheria za utumishi wa umma kutokana na uzembe na matokeo yake kuleta matokeo mabovu katika Taasisi.

"Tufanye kazi kwa bidii na kwa uaminifu kazini kwa kufuata misingi Mikuu ya Uadilifu, ikiwemo uwajibikaji na uaminifu," amesema Dkt. Mhina

Aidha, Dkt. Mhina amesema mtumishi anapaswa kutunza siri za ofisi kwa kutotumia taarifa za Serikali visivyo sahihi au bila idhini ya Utawala kwani Kanuni zinawataka kutunza taarifa kwa siri.

Vilevile, Dkt. Mhina ameitaka Menejimenti ya LITA kuwajengea watumishi wao uwezo na kuhakikisha wana utendaji mzuri kazi, na wanakuwa na uadilifu kwa kuzingatia Sheria na kanuni na Taratibu za Utumishi wa umma.

Dkt. Mhina amewapongeza LITA kwa mpangilio mzuri wa kampasi ambao zimekuwa zinatoa fursa mbalimbali zinazoonekana kwa wafugaji. 

Halikadhalika, Dkt. Mhina amesema bado kuna jukumu kubwa la kutoa mafunzo ya mifugo kwa wafugaji kwani chuo hakiwezi kuendelea kama hakiwekezi kwenye Miundombinu na ushirikishwaji wa jamii kwenye kutoa Mafunzo ya Mifugo.

Pia, Dkt. Mhina, ameipongeza Kamati ya Wajumbe wa Baraza Kuu LITA kwa kuendelea kujenga Vyuo vingine katika sehemu mbalimbali na amewataka Baraza kuisaidia Menejimenti katika kubuni Miradi mingine, ikiwa pamoja na kupima kama Mipango inaleta tija ambayo itaenda kufanya mabadiriko makubwa katika Taasisi baada ya miaka kadhaa ili kufanya maboresho makubwa zaidi.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene amesema wamepata nasaha kubwa kutoka kwa Mgeni Rasmi, na kuahidi kushirikishana katika Mipango yote ambayo imepangwa kwa Mwaka ujao wa fedha.

Dkt. Mwambene amesema wataendelea kuzingatia Maadili ya Utumishi wa Umma kwa kutekeleza Majukumu waliopewa na Serikali na kuwajibika ili kuleta matokeo chanya kwa Taasisi na nchi nzima.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina, akitoa Hotuba katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene, akielezea Historia ya Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) pamoja na Mafanikio na Changamoto za Taasisi hiyo, katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) ambaye ni Naibu Mkuu wa Chuo Taaluma Utafiti na Ushauri LITA, Dkt. Anna Ngumbi, akitoa neno la shukrani kwa Mgeni Rasmi (hayupo pichani), katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina (katikati) na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), Dkt. Pius Mwambene (kushoto), wakiimba wimbo wa  Mshikamano Daima wa Wafanyakazi wa LITA, katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma, kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi.

Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Samwel Mdachi na Mkurugenzi  Msaidizi wa Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bi. Josephine Temihango (wa kwanza kulia), wakipitia Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Taasisi  hiyo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Picha ni baadhi ya Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), wakiwa  katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) la Baraza hilo, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.

Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, ambaye ni  Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Charles Mhina (katikati waliokaa), akiwa katika picha ya pamoja Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi Wakala wa Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA), katika Kikao cha Utoaji Taarifa za Mkutano wa Kumi na mbili (12) wa Baraza Kuu la Wafanyakazi hao wa LITA, kilichofanyika katika Ukumbi wa St. Gaspar, Aprili 4, 2025, Dodoma.















Alhamisi, 3 Aprili 2025

MELI YA UTAFITI WA UVUVI BAHARINI YAPOKELEWA VISIWANI ZANZIBAR

Na Hamis Hussein, Zanzibar

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepokea Meli ya Utafiti wa Uvuvi kutoka Nchini  Norway kwa lengo la kufanya utafiti wa wingi wa  Rasilimali za Uvuvi na Mfumo wa Ikolojia.

Akizungumzia ujio wa Meli hiyo Wakati wa Mapokezi yaliyofanyika Leo Aprili 02, 2025  katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja Visiwani Zanzibar, Waziri wa Uvuvi na Uchumi wa Buluuu Zanzibar, Mhe. Shaaban Ali Othman amesema Meli hiyo ijulikanayo kwa jina la Dr. Fridjof Nansen  itaisaidia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  kujua uelekeo mpya wa Sekta ya uchumi wa Buluu na kuwasaidia wavuvi kujua  maeneo ambayo samaki wanapatikana kwa uhakika.

"Ujio wa Meli hii kwetu sisi kama Tanzania na  kama Zanzibar  inatusaidia  kujua uhalisia wa rasimali za uvuvi zilizomo katika  Bahari yetu, Serikali imeshafanya uwekezaji mkubwa kupitia baharini, kwahiyo taarifa za kitaalam na takwimu zitazopatikana zitawasaidia pia wavuvi wetu" alisema Mhe. Shaabani Ali Othman.

Kwa upande wake Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede kwa niaba ya Katibu Mkuu Prof. Riziki Shemdoe amesema Serikali itaendelea kusimamia tafiti  zinazofanywa na wataalam kuhusu rasilimali za baharini ili  zijikite kwenye kujua wingi wa rasilimali za uvuvi zinazopatikana kwenye Bahari.

"Tutafurahi kuona utafiti uliopita ulionyesha kulikuwa na ongezeko la rasilimali tulizonazo ndani ya maji yetu lakini tunahimiza utafiti utakaofanyika awamu inayofuata mwezi Oktoba ujikite  katika kujua wingi wa rasilimali tulizonazo kwenye Bahari yetu" alisema Dkt. Mhede.

 Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI), DKt. Ismael Kimirei amesema utafiti wa awamu hii unaoanza kufanyika  Alhamisi ya Aprili 03, 2025 utaanzia kwenye maji ya Bahari ya Hindi upande wa Kusini mwa Mtwara hadi mwisho wa Pemba huku ukitarajiwa kutumia Siku 19  kwa kukusanya taarifa za wingi wa Samaki, mtawanyiko wake na aina mpya za Samaki zitakazopatika.

Aidha, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani FAO Nchini Tanzania Dkt. Nyabenyi Tipo  amewahimiza wadau kushirikiana na Serikali  kufanya mijadala  ya kuimarisha uhai wa  Viumbe maji vinavyopatika kwenye Bahari ya Hindi ili viweze kuinua Uchumi wa buluu na  maisha ya Wavuvi kwa ujumla.

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi- Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman (Katikati, Waliokaa), akiwa kwenye picha ya pamoja na Viongozi wa Wizara za Mifugo na Uvuvi (JMT) na Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi (SMZ), Mkurugenzi Mkazi wa FAO-Tanzania na watafiti mbalimbali mara baada ya kutembelea maeneo mbalimbali ndani ya meli eneo la Bandari ya Malindi, ikiyopo Mjini Unguja, Zanzibar Aprili 02, 2025.
Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi-Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman akizungumza wakati wa mapokezi ya Meli ya Utafiti wa Rasilimali za Uvuvi Baharini iitwayo Dr. Dr. Fridtjof Nansen, Hafla iliyofanyika Bandari ya Malindi Mjini Unguja, Zanzibar, Aprili 2, 2025.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Uvuvi) Dkt. Edwin Mhede kwa niaba ya Katibu Mkuu Prof. Riziki Shemdoe akielezea jinsi serikali ya Tanzania itakavyoendelea kusimamia Tafiti za  Uvuvi wakati wa mapokezi ya Meli ya Utafiti wa Rasilimali za Uvuvi Baharini inayojulikana kama  Dr. Fridtjof Nanseni.  Hafla ya mapokezi ya meli hiyo imefanyika katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja, Zanzibar, Aprili 2, 2025.

Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi -Zanzibar Mhe. Shaaban Ali Othman (Watatu Kushoto ) akisikiliza maelezo kutoka kwa mtafiti wa Meli ya Utafiti ya Dr. Fridtjof Nansen wakati alitembelea maeneo mbalimbali ndani ya meli hiyo ili kujifunza namna utafiti unavyofanyika kwa kutumia vifaa vya kisasa., Hafla ya mapokezi ya meli hiyo imefanyika katika Bandari ya Malindi Mjini Unguja, Zanzibar, Aprili 2, 2025.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania Dkt. Ismael Kimirei akizungumzia juu ya Tafiti za Viumbe maji wa baharini na tija itakayopatikana katika kuimarisha uchumi wa Buluu wakati wa mapokezi ya Meli ya Utafiti ya Dr. Fridjof Nansen hafla iliyofanyika Bandari ya Malindi, Mjini Unguja, Zanzibar Aprili 02, 2025.

Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kikimo Duniani FAO Nchini Tanzania Dkt. Nyabeti Tipo akizungumza wakati wa mapokezi ya Meli ya Utafiti ya Dr. Fridtjof Nanseni, Hafla iliyofanyika Bandari ya Malindi Mjini Unguja, Zanzibar, Aprili 2, 2025.

Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Zanzibar (ZAFIRI)  Dkt. Zakaria Hamis akitoa neno la Ufunguzi katika hafla ya kupokea Meli ya Utafiti ya Dr. Fridjof Nansen.  Hafla hiyo, imefanyikakatika Bandari ya Malindi, Mjini Unguja, Zanzibar Aprili 02, 2025.

Mkurugenzi wa Uvuvi kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Prof. Mohamed Shekh akitoa neno la Shukran kwa Shirika la FAO, Serikali ya Norway kwa kuwezesha  ujio wa Meli ya Utafiti ya Dr. Fridjof  Nansen Wakati wa Hafla ya Mapokezi ya Meli hiyo  iliyofanyika Bandari ya Malindi, Mjini Unguja, Zanzibar Aprili 02,  2025.