Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2024

DKT KIJAJI AIAGIZA NARCO KUZALISHA MBEGU ZA MIFUGO, MALISHO KWA WINGI

Picha
Na. Stanley Brayton ◼️Ataka visima 6  vya maji NARCO kukamilishwa Kabla ya  January 5, 2025  Waziri wa Mifugo na  Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ameiagiza Kampuni ya Ranchi za Taifa NARCO iliyopo Kongwa Jijini Dodoma Kuongeza wigo wa Uzalishaji wa Mbegu Bora za  Mifugo na Malisho itakayoongeza upatikanaji wa Nyama nchini na Kukuza uchumi wa Wafugaji. Dkt. Kijaji ametoa maagizo hayo Leo Desemba 17, 2024 Wakati wa Ziara yake kwenye Kambuni ya Ranchi za Taifa NARCO na kuahidi kurudi Januari 5, 2025 ili kuona utekelezaji wa maagizo hayo. " NARCO Mnajukumu la kuzalisha mbegu bora za aina Mbalimbali, Watanzania wanahitaji mifugo inayouzika kwa urahisi  hapa ndani ya nchi na  Kimataifa tunataka kila mfugaji akiuza Ng'ombe apate Milioni Nne hivyo nawataka Mzalishe mbegu Bora kwaajili wafugaji wetu" amesema Dkt. Kijaji. Kuhusu uzalishaji wa Mbegu za Malisho Dkt Kijaji amemwagiza Mkurugenzi wa Uzalishaji na Maendeleo ya  Masoko Stephen Michael  kushirik...

DKT. KIJAJI KUENDELEZA ALIPOISHIA ULEGA KUKUZA SEKTA ZA MIFUGO NA UVUVI

Picha
Na. Stanley Brayton  ◼️ Awahimiza wataalam ushirikiano  Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesema katika kuendeleza na kukuza sekta za Mifugo na Uvuvi ataanzia pale alipoishia mtangulizi wake Mhe. Abdallah Ulega  ili kuendelea kuzifanya sekta hizo kuwa na mchango mkubwa zaidi kwenye pato la taifa. Dkt. Kijaji amesema hayo Disemba 15, 2024 wakati wa makabidhiano ya nyaraka za ofisi baina yake na Mtangulizi wake huyo katika hafla  fupi iliyofanyika Makao Makuu ya wizara, Mji wa Serikali Mtumba Jijini Dodoma. “Kaka yangu, Mhe. Ulega umefanya kazi kubwa ya kuipaisha wizara hii na mimi nitaendelea kujifunza kutoka kwako ili niweze kukimbia na kasi ambayo Mhe. Rais anaitaka” Amesema Mhe. Dkt. Kijaji. Mhe. Dkt. Kijaji ameongeza kuwa dhamira yake ni kuona sekta za Mifugo na Uvuvi zinakuwa miongoni mwa sekta muhimu katika ustawi wa uchumi wa  Wananchi na taifa kwa ujumla huku akiwahimiza wataalamu kushirikiana hasa katika kuwahudumia wafugaji na Wavuvi am...