Nav bar

Jumapili, 27 Agosti 2023

WAFUGAJI WA SAMAKI WAHIMIZWA KUKITUMIA KITUO CHA MWAMAPULI

Wafugaji wa samaki Kanda ya Magharibu wamehimizwa kukitumia Kituo cha Mwamapuli kwa ajili ya kupata elimu ya ufugaji wa kisasa na kibiashara.

 

Hayo yamesemwa leo (07.08.2023) na Wilbard Mapindo ambaye ni Afisa Uvuvi Msaidizi kutoka Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji Mwamapuli kilichopo Wilayani Igunga mkoa wa Tabora. Mapindo amesema kituo hicho kinafanya kazi kubwa ya utoaji elimu kwa wafugaji wa samaki wa Kanda ya Magharibi na hata Kanda nyingine za jirani.

 

Wafugaji wa samaki wamekuwa wakienda kutembelea kituoni hapo kwa lengo la kupata elimu ya ufugaji bora wa samaki ambapo pia wamekuwa wakitakuliwa changamoto mbalimbali ambazo wamekuwa wakikutana nazo katika shughuli ya ufugaji wanayoifanya.

 

Pia amesema kwa sasa kituo kimezidi kuimarika ambapo uzalishaji wa vifaranga vya samaki umeongezeka hivyo amewatoa hofu wafugaji wa samaki kuwa wafike kituoni hapo kwa ajili ya kununua vifaranga ambavyo bei yake pia ni Rafiki kwa mtu yeyote.

 

Vilevile Mapindo amewashi wafugaji wa samaki kuhakikisha wanawatumia Maafisa Ugani waliopo katika maeneo yao kwa ajili ya kupata msaada wa kitaalam pale wanapokutana na changamoto yoyote kwenye ufugaji.

 

Naye Mussa Budaga ambaye ni mmoja wa wafugaji wa samaki kutoka Wilaya ya Kaliua mkoani Tabora amesema kuwa wananufaika sana na uwepo wa Kituo hicho cha Mwamapuli kwa kuwa kinawasaidia kupata elimu ya ufugaji bora wa samaki.

 

Budaga amesema kuwa ufugaji wa samaki una faida kuwa ikiwa ni pamoja na lishe bora na kujiongezea kipato, hivyo amewasihi wananchi kuanza kufuga samaki kwa kuwa uwekezaji wake unalipa endapo taratibu zinazotolewa na wataalam wa ufugaji samaki zitafuatwa.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni