Nav bar

Jumatatu, 26 Juni 2023

FETA YATAKIWA KUTANUA WIGO WA MASHIRIKIANO KATIKA KUTOA MAFUNZO

Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA) imetakiwa kuongeza wigo wa mashirikiano katika kutoe elimu ya uvuvi.

 

Hayo yamesemwa na Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Prof. Mohamed Sheikh wakati akifunga mafunzo ya siku 30 ya kuwajengea uwezo wakaguzi wa mazao ya samaki juu ya usalama, ubora na taratibu za ukaguzi kutoka nchini Somali, mafunzo ambayo yaliyofanyika kwenye ukumbi wa ofisi ya Chuo cha Mafunzo ya Uvuvi Kampasi ya Mbegani wilaya ya Bagamoyo Mkoani Pwani.

 

Prof. Sheikh amesema kuwa FETA inatakiwa kuongeza wigo wa mashirikiano na nchi mbalimbali kwani zipo rasilimali nyingi na wataalam wapo wa kutosha hivyo haitakiwi wataalam kujifungia wenyewe badala yake wajitokeze na kuhakikisha wanatoa mafunzo ili kuongeza utaalam kwenye utekelezaji wa shughuli za uvuvi.

 

Vilevile amewasihi kuendelea kutafuta vyanzo mbalimbali vya fedha kwa ajili ya kuendesha mafunzo hayo kwa watu wa ndani na nje ya nchi hasa wanaijishughulisha na shughuli za uvuvi.

 

Wataalam wa uvuvi kutoka Somalia wamekuwa wakishiriki mafunzo hayo hapa nchini kwa lengo la kuongeza uwezo katika kusimamia rasilimali za uvuvi na kuhakikisha kuwa kuna kuwa na uvuvi endelevu nchini kwao.

 

Prof. Sheikh amesema upo umuhimu mkubwa katika kuhakikisha mazao ya bahari yanakuwa na ubora unaotakiwa, hivyo ameitaka FETA kuhakikisha inaendela kuhamasisha na kutoa mafunzo hayo kwa washiriki kutoka nchi mbalimbali.

 

Vilevile amelishukuru Shirika la Kilimo na Chakula Duniani (FAO) kwa kuwezesha kufanyika kwa mafunzo hayo ambapo ameyaomba na mashirika mengine kuiga mfano huo ili kuwezesha mafunzo hayo kuwafikia washiriki wengi zaidi.

 

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA), Dkt. Semvua Mzighani amesema kuwa mafunzo yanayotolewa chuoni hapo msisitizo mkubwa huwa ni kwenye kufanya mafunzo kwa vitendo hivyo ni matarajio yake kuwa watakaporejea nchini kwao watakwenda kutekeleza yale waliyofundishwa kwa vitendo kitu ambacho kitawaongezea ujuzi zaidi na kusaidia kutoa elimu kwa wengine.

 

Vyuo vya vyao vinatoa mafunzo ya uhandisi katika maji, ubora wa samaki, uvuvi na ubaharia, ukuzaji viumbe maji, mazingira na rasilimali za bahari, sayansi ya bahari na menejimenti ya bahari.

 

Akiongea kwa niaba ya wanafunzi wengine Rais wa wanafunzi hao kutoka chuo cha Uvuvi nchini Somalia bwana Elm A. Mohamed alisema kuwa nchi zetu vyema zikashirikiana katika rasilimali zetu kwani zinafanana hasa ukanda wa bahari pamoja na ufugaji vilevile tushirikiane kati Nyanja za utamaduni kwani utamaduni wa watanzania ni mzuri sana.

 

Mafunzo hayo ya mwezi mmoja yameanza tarehe 12/05/2023 na kumalizika tarehe 13/06/2023 ambapo pamoja na mafunzo washiriki wamepata fursa ya kujifunza Kiswahili na Tamaduni za Kitanzania.



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni