Nav bar

Ijumaa, 19 Mei 2023

WATAALAM WA WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI WAMTEMBELEA MFUGAJI BW. JEREMIAH TEMU JIJINI DODOMA


 Mfugaji Bw. Jeremiah Temu akionyesha namna ya kukata malisho kwa kutumia mashine nyumbani kwake Mpamaa jijini Dodoma kwa wadau na wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi walipoenda kujifunza, Mei 17,2023

Mkurugenzi Msaidizi wa Maeneo ya Malisho kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Bw. Gabriel Bura (kulia) akisambaza malisho  ambayo yamekatwa kwa kutumia mashine kwenye eneo lililoandaliwa  kwa ajili ya kutengeneza saileji nyumbani kwa mfugaji  Bw. Jeremiah Temu Mpamaa jijini Dodoma,  Mei 17,2023

Sehemu ya vijana wakishindilia malisho yanayoandaliwa kwa ajili ya kutengeneza saileji kwa kutumia pipa la maji kwenye eneo lililoandaliwa ikiwa ni hatua moja wapo ya maandalizi nyumbani kwa mfugaji Mpamaa jijini Dodoma,  Mei 17,2023.

Mkurugenzi Msaidizi wa Maeneo ya Malisho kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Bw. Gabriel Bura  (kushoto) akionyesha sehemu malisho yanapoanzia kukatwa na umuhimu wake kwa watendaji kutoka Wizara hiyo wakati walipotembelea shamba la mfugaji Bw. Jeremiah Temu lililopo Mpamaa jijini Dodoma Mei 17,2023

Mfugaji Bw. Jeremiah Temu (wa nne kutoka kulia) akitoa maelezo kwa wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi walipomtembelea nyumbani kwake kwa lengo la kujifunza namna ya kupanda malisho na kutengeneza saileji kwa ajili ya mifugo Mpamaa jijini Dodoma Mei 17,2023

Sehemu ya malisho aina ya junkao yaliyopandwa nyumbani kwa mfugaji Bw.  Jeremiah Temu  Mei 17,2023 Mpamaa jijini Dodoma.

Mfugaji Bw. Jeremia Temu (kushoto) akitoa maelezo ya maana ya saileji na faida yake kwa mifugo, kwa wadau na wataalam kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi  waliomtembelea nyumbani kwake Mpamaa jijini Dodoma kwa lengo la kujifunza, Mei 17,2023


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni